Benki Kuu ya Sudan siku ya Jumatano iliamua kuruhusu makampuni ya kuuza dhahabu nje ya nchi, baada ya kupiga marufuku hatua hiyo Septemba 2025.

Uamuzi wa Benki Kuu, uliotolewa mnamo Septemba 15, ulisababisha mzozo kati ya taasisi za serikali na wauzaji bidhaa nje ambao waliukanusha.

Benki hiyo ilisema katika taarifa kwamba sasa “inaruhusu usafirishaji wa dhahabu nje ya nchi na mtu yeyote baada ya kutimiza taratibu za usafirishaji, mradi inauzwa nje kulingana na bei ya soko la kimataifa.”

Ilibainisha kuwa malipo ya mauzo ya dhahabu lazima yakusanywe kupitia malipo ya awali au barua za mkopo, ambayo haitakiwi kujumuisha masharti yanayohusiana na kubadilisha bidhaa nje ya nchi, na thamani ya mapato ya mauzo ya nje kurejeshwa ndani ya siku 30 kuanzia tarehe ya usafirishaji.

Benki Kuu iliruhusu wasafirishaji wa dhahabu kutumia mapato yao ya mauzo ya nje na pia iliruhusu kuuzwa kwa benki yoyote au Benki Kuu.

Uzalishaji wa dhahabu wa Sudan katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wa serikali kuu ulifikia tani 53 katika miezi tisa ya kwanza ya mwaka huu, wakati mapato ya mauzo ya nje yalikuwa yasiyopungua dola milioni 909, na kusababisha vyombo kadhaa kuchunguza tofauti za bei.

Marukufu ilihusisha nini?

Chini ya marufuku iliyowekwa hapo awali Benki kuu ya Sudan iliwajibisha wauzaji dhahabu nje ya nchi kuzingatia udhibiti uliotolewa na Wizara ya Viwanda, Wizara ya Madini, Shirika la Viwango na Hali ya hewa la Sudan, na Kampuni ya Sudan Gold Refinery.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *