Ni wakati wa wakuu wa nchi za Afrika Magharibi kutoa tathmini zao. Katika salamu zao za Mwaka Mpya, Rais wa Côte d’Ivoire Alassane Ouattara na Rais wa Togo Faure Gnassingbé wamesisitiza utulivu wa kitaasisi na mwendelezo wa madaraka. Katika nchi za Sahel, zinakabiliwa na ukosefu wa usalama unaoendelea, viongozi wa Mali na Burkina Faso wamesifu hasa kujitolea kwa vikosi vya ulinzi na usalama.

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Nchini Côte d’Ivoire, rais Ouattara alikuwa wa kwanza kuzungumza mapema jioni. Alassane Ouattara alitoa shukrani zake kwa kuchaguliwa kwake tena kwa muhula wa nne. Aliwapongeza raia wake kwa uchaguzi aliouelezea kama “uwazi na wa kuaminika,” ingawa wagombea kutoka vyama viwili vikuu vya upinzani walizuiliwa kugombea.

Mwaka mpya unamaanisha salamu za Mwaka Mpya. Huko Abidjan, wakazi wanatoka katika mwaka wa uchaguzi ambapo kulisuhudiwa uchaguzi wa rais na wa wabunge. Akili bado zinalenga umuhimu wa kuhifadhi utulivu na mshikamano wa kijamii. Mwandishi wetu wa kitengo cha RFI katika kanda ya Afrika Bineta Diagne amekusanya maoni ya Waivory Coast katika mitaa ya Abidjan, saa chache tu kabla ya Mkesha wa Mwaka Mpya.

Matamanio yangu kwa Côte d’Ivoire ni matakwa ya kwanza kabisa ya amani, mshikamano, uelewano, na ustawi katika nyanja zote.

Hisia kama hiyo imeripotiwa nchini Togo, ambapo Faure Gnassingbé, akiwa madarakani kwa miaka 20, alijaribu kuhalalisha marekebisho yake ya katiba. Kwake, “katika Jamhuri, kuna mambo ambayo lazima yabaki thabiti.” “Mwendelezo wa Serikali na taasisi zake ni muhimu. Ndiyo maana nilibaki mkuu wa serikali,” aliongeza.

Nchini Dakar, Rais Bassirou Diomaye Faye alitoa salamu zake za Mwaka Mpya, huku vuguvugu la kiraia Ye’en a marre (Inatosha Inatosha) zikimpa changamoto kuhusu mageuzi ya haki na matumizi ya serikali. Katika tathmini yake, mkuu wa nchi alibainisha kwamba kupunguzwa kwa kiasi kikubwa kwa matumizi ya umma tayari kumeanzishwa na kutangaza kwamba mageuzi ya haki yatafanyika mwaka wa 2026.

Mwaka uliopita umekuwa wakati wa ukweli kwa nchi yetu. Umefichua ukosefu wa usawa mkubwa.

Kwa upande wa Shirikisho la mataifa ya Sahel, yaliyokumbwa na ukosefu wa usalama, Rais wa Mali Assimi Goïta na Rais wa Burkina Faso Ibrahim Traoré, wote walitoa heshima kwa vikosi vya ulinzi na usalama. Rais wa Mali alisifu “ushujaa” wa wanajeshi na wasafirishaji wote wa raia waliohakikisha usambazaji wa bidhaa kwenda Mali “kwa kuhatarisha maisha yao.” Kuhusu Ibrahim Traoré, alitangaza kwamba amerejesha udhibiti wa vijiji kadhaa, haswa katika mkoa wa Nakambé.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *