
Kulingana na takwimu za nchini Syria, raia zaidi ya 3,000 wameondoka katika maeneo yao kutokana na mashambulizi ya magaidi wa YPG.
Vurugu hizi zimelazimisha uongozi wa mkoa huko Aleppo kutangaza kuendelea kufungwa kwa shule za umma na binafsi pamoja na vyuo vikuu kwenye mji huo siku ya Alhamisi.
Machi 10, ofisi ya rais wa Syria ilitangaza kutiwa saini kwa makubaliano ya kujumuisha YPG katika taasisi za serikali, kusisitiza kuhusu umoja wa nchi hiyo na kukataa majaribio yoyote ya kuleta mgawanyiko.
Mamlaka nchini Syria zinasema kuwa miezi kadhaa tangu wakati huo, YPG haijaonesha juhudi za kutekeleza yaliyokuwemo kwenye makubaliano hayo.
Serikali ya Syria imezidisha juhudi za kuhakikisha usalama kote nchini tangu kuondolewa madarakani kwa utawala wa Bashar al Assad Disemba 8 2024, baada ya kuwepo uongozini mwa miaka 24.