Ali Muhammad Ali Abd-Al-Rahman, anayejulikana pia kama  Ali Kushayb , alipatikana na hatia ya makosa mengi ya uhalifu ikiwa ni pamoja na ubakaji, mauaji na mateso yaliyotekelezwa kati ya Agosti 2003 na Aprili 2004 vilivyofanywa wakati wa mashambulizi ya kikatili huko Darfur , lakini mwenyewe alikana mashtaka hayo.

Joanna Korner, Jaji kiongozi wa ICC yenye makao yake mjini The Hague Uholanzi amesema mahakama hiyo inao ushahidi wa kutosha kuwa mshtakiwa aliyekuwa mkuu wa wanamgambo wa Janjaweed huko nchini  Sudan  ana hatia kwa makosa yanayomkabili huku akisisitiza kuwa hukumu ya adhabu yake itatolewa hapo baadaye.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *