Nchini Mali, maafisa kumi na mmoja wa vyeo vya juu, wakiwemo majenerali wawili, wamefutwa kazi jeshini. Uamuzi huo ulitolewa kwa agizo mnamo Oktoba 8, 2025, na rais wa mpito, Jenerali Assimi Goïta. Wanajeshi hawa walikamatwa mwezi Agosti, wakishutumiwa kwa “njama” na “kujaribu kuhatarisha usalama wa taasisi” pamoja na maafisa wa kijasusi wa Ufaransa.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Chini ya miezi miwili baada ya kukamatwa kwao, na bila hata kuhukumiwa, kutimuliwa kwa askari kumi na mmoja ni adhabu ya kinidhamu, si uamuzi wa mahakama.

Majenerali Abass Dembélé, gavana wa zamani wa Mopti, na Néma Sagara, mwanamke katika jeshi la anga, ndio wanaojulikana zaidi, wote wanajulikana sana ndani ya jeshi la Mali. Maafisa sita wa vyeo vya juu (Luteni kanali), maafisa wawili (kepteni), na sajenti mmoja wanakamilisha orodha hiyo. Picha za baadhi yao zilionyeshwa mwezi Agosti na kituo cha televisheni cha serikali ORTM. Mamlaka ya mpito ilidai kuwa ilizuia jaribio la mapinduzi.

“Mbinu potovu”

“Hizi ni tuhuma zilezile zinazotolewa dhidi ya wote waliofukuzwa kazi,” kimethibitisha chanzo cha usalama cha Mali, kikielezea “mbinu potovu” ya mamlaka ya mpito, kulingana na chanzo hicho. Msimu huu wa joto, askari kadhaa walikamatwa na usalama wa taifa wakati wa operesheni kubwa.

Je, uchunguzi uliotangazwa umehitimisha kuwa kulikuwa na njama ya kweli ya kuhatarisha usalama wa taifa? Hakuna ushahidi uliowekwa wazi. Waangalizi wengi wa Mali wanaamini kuwa utawala wa sasa unajaribu kuzima hisia zozote za upinzani, hata kama ni madogo, ndani ya jeshi. “Itaongeza idadi ya wanajeshi waliokatishwa tamaa,” kimesema chanzo hicho cha usalama cha Mali.

DGSE

Raia mmoja wa Ufaransa pia alikamatwa huko Bamako mnamo Agosti, akishutumiwa kushiriki katika “njama” hii. Uanachama wa Yann Vézilier katika DGSE ulijulikana kwa mamlaka ya mpito. Kukamatwa kwake-kutokana na “tuhuma zisizo na msingi,” kulingana na Paris-pia kulisababisha kuvunjwa kwa ushirikiano wa kupambana dhidi ya ugaidi kati ya Mali na Ufaransa mwezi uliopita, ambao idara za kijasusi ziliendelea kubadilishana habari licha ya mvutano wa kidiplomasia.

Raia wa Ufaransa na wanajeshi wa Mali waliokamatwa miezi miwili iliyopita bado wanazuiliwa katika eneo lisilojulikana.

© David Baché

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *