Katika Afrika ya Kati, salamu za Mwaka Mpya wa 2026 ni fursa ya kujadili uchaguzi. Nchini Gabon na Cameroon, Brice Clotaire Oligui Nguema na Paul Biya wamesisitiza uhalalishaji wa mamlaka yao kupitia sanduku la kura, la kwanza baada ya mapinduzi ya mwaka 2023, la mwisho kwa muhula wa nane uliokuwa ukigombewa. Nchini Kongo, Denis Sassou Nguesso ametoa wito wa uchaguzi wa urais wa amani mnamo mwezi Machi 2026.

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Kwa Jenerali Brice Clotaire Oligui Nguema, 2025 ulikuwa mwaka wa kuhalalisha mapinduzi yake ya mwaka 2023 nchini Gabon kupitia uchaguzi. Aliwapongeza raia wa Gabon kwa “ujio wa Jamhuri ya Tano,” kufuatia kufanyika kwa uchaguzi wa wabunge, wa maseneta, na urais, ambao alishinda kwa zaidi ya 90% ya kura.

Kuanzia kura ya maoni ya kikatiba hadi uchaguzi wa wa maseneta, ikiwa ni pamoja na uchaguzi wa urais na wa wabunge, umechangia, kupitia hisia zeko kubwa za uzalendo, katika ujio wa Jamhuri yetu ya Tano.

Nchini Cameroon pia, tunaangalia nyuma uchaguzi wa urais, na picha inayoendelea ya maandamano yaliyokandamizwa kwa nguvu. Mwishoni mwa mwezi Oktoba, Paul Biya, aliye madarakani tangu mwaka 1982, alichaguliwa tena kwa mara ya nane kama mkuu wa nchi. Katika hotuba yake ya Mwaka Mpya, rais huyo mzee zaidi duniani aliwashukuru raia kwa “imani yao” na kutangaza kwamba ataunda serikali katika siku zijazo.

Hakuna matangazo makubwa yaliyotolewa kuhusu mgogoro wa baada ya uchaguzi ulioitikisa Cameroon baada ya matokeo ya uchaguzi wa urais, lakini ahadi ilitolewa ya kuunda serikali mpya katika siku zijazo, anaripoti mwandishi wetu huko Yaoundé, Richard Onanena.

Siasa, uchumi, miundombinu, nishati, na ajira kwa vijana. Kwa karibu dakika 20 Paul Biya alirejelea mada ambazo alizungumzia wakati wa kuapishwa kwake.

Nchini Chad, Rais Mahamat Idriss Deby, wakati wa hotuba yake ya Mwaka Mpya mnamo Desemba 31, aliwasihi mahakimu kurejesha taswira ya mfumo wa haki wa Chad, ambao mara nyingi hushutumiwa kuwa chini ya mamlaka ya kisiasa na umejaa ufisadi, kama rais wa Chad mwenyewe alivyopendekeza.

Kwa kujitolea kwa dhati kwa mgawanyo mzuri wa madaraka na uhuru wa mahakama kupitia kujiondoa kwetu kutoka Baraza Kuu la Mahakama, lengo letu pekee ni kuimarisha haki kama msingi wa taifa letu.

Kuhusu Denis Sassou Nguesso, ambaye amekuwa madarakani nchini Congo-Brazzaville kwa miaka 40, alizungumzia kwa kina kuhusu uchaguzi ujao wa rais mnamo mwezi Machi 2026. Aliuelezea kama tukio “nyeti na lenye maamuzi sawa”, akitaka uchaguzi wa amani. Mnamo Desemba 30, aliteuliwa kwa kauli moja kama mgombea wa Chama tawala cha PCT.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *