
Shirikisho la soka Barani Afrika (CAF) limeshtumu vikali kile walichokitaja kuwa ‘‘tabia isiyokubalika” ya wachezaji na maafisa wakati wa mechi mbili za robo fainali kwenye AFCON 2025 nchini Morocco, na imeanzisha uchunguzi rasmi kuhusu matukio hayo.
Katika taarifa siku ya Jumatatu, CAF inasema imetathmini ripoti ya mechi na ushahidi wa video zikidhihirisha uwezekano wa utovu wa nidhamu wakati wa michuano ya robo fainali kati ya Cameroon na Morocco, na Algeria na Nigeria.
Nchi wenyeji Morocco ilishinda 3–2 dhidi ya Cameroon mechi ya robo fainali, iliyomalizika kwa uhasama.
Wachezaji kadhaa wa timu zote mbili walikabiliana uwanjani, huku maafisa wakiwatenganisha wakati timu zikitoka uwanjani.
Hisia kali baada ya mechi
Katika mechi nyingine ya robo fainali, Nigeria iliishinda Algeria 2–0, mechi ambayo Algeria ililalamika, ikidai kuwa matokeo yalichochewa na uamuzi mbaya, ikiwemo kilio cha penati cha Algeria ambacho hakikusikilizwa.
Hasira zilitokana na wachezaji na maafisa wa Algeria, na makabiliano yakazuka punde tu baada ya mechi. Maafisa wa usalama na waamuzi waliingilia kati kutuliza hali huku kukiwa na vuta nikuvute karibu na maeneo ya mabenchi ya ufundi.