Kulingana na kamandi ya jeshi la Marekani, mashambulizi haya yaelenga ulinzi wa anga wa Iran, vituo vya udhibiti, na mitambo ya rada karibu na Mlango-Bahari wa Hormuz.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Hapo awali, siku ya Jumanne jioni, Marekani ilizungumzia kuhusu mwitikio sawia baada ya helikopta ya Apache kuharibiwa siku ya Jumatatu jioni na ndege isiyo na rubani ya Iran, bila kusababisha majeruhi wowote. Lakini jibu la Marekani linaonekana kuwa kali sana. Na bila shaka ndiyo maana taarifa ya pili ilitolewa siku ya Jumanne, wakati huu ikirejelea kwa maneno mapana zaidi “mashambulizi ya hivi karibuni dhidi ya vikosi vya Marekani na dhidi yameli za kibiashara zinazopita katika eneo hilo.”

Donald Trump alichagua kutumia nguvu, lakini kwa mara nyingine tena anaonekana amebadilisha mawazo yake, kwani katika mahojiano na Gazeti la Wall Street Journal, alipuuza tukio lililohusisha helikopta hiyo, akibainisha kwamba marubani wako salama salimini.

Marekani imesema mashambulizi yake ni “jibu” kwa kudunguliwa kwa helikopta hiyo, tukio ambalo Rais Donald Trump alilitaja kuwa lilifanywa na Iran, wakati IRGC likiyaita mashambulizi ya Marekani kuwa “ya kikatili”.

Tukio hilo lilitokea baada ya wafanyakazi wawili wa helikopta ya Marekani ya Apache kuokolewa na droni ya majini ya Marekani siku ya Jumatatu, ikiwa ni mara ya kwanza kwa jeshi la Marekani kutumia aina hiyo ya chombo katika operesheni ya uokoaji.

Maafisa wa Marekani walisema Iran ilitumia droni kushambulia helikopta hiyo, lakini bado haijathibitishwa kama shambulio hilo lilikuwa la makusudi. Shirika la habari la Mehr liliripoti kuwa Iran haijakiri kuhusika.

Centcom ilisema ndege za kivita za Marekani zilishambulia mifumo ya ulinzi wa anga ya Iran, vituo vya udhibiti wa ardhini, na rada karibu na Mlango wa Hormuz.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *