Kiongozi wa upinzani wa Venezuela na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, María Corina Machado, atakutana na Rais Donald Trump siku ya Alhamisi, Ikulu ya Marekani imethibitisha.

Ziara hiyo inafanyika wiki chache tu baada ya Rais wa Venezuela Nicolás Maduro kukamatwa huko Caracas na vikosi vya Marekani. Lakini Trump alikataa kumuidhinisha Machado, ambaye harakati zake zilidai ushindi katika uchaguzi uliokuwa na ushindani mkubwa wa 2024, kama kiongozi wake mpya.

Badala yake Marekani ilimuunga mkono Delcy Rodríguez, makamu wa rais wa zamani wa Maduro.

Machado alisema wiki iliyopita alisema anatumai kumshukuru Trump binafsi kwa hatua aliyochukua dhidi ya Maduro na angependa kumtunuku Tuzo ya Nobel.

Trump aliiita hatua hiyo “heshima kubwa”, lakini Kamati ya Nobel baadaye ilifafanua kwamba haiwezi kukabidhiwa mtu mwingine.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *