Rais wa Tume ya Ulaya, Ursula von der Leyen, alisema Jumatano kwamba Umoja wa Ulaya (EU) unapanga kugawanya msaada wa kifedha wa…Rais wa Tume ya Ulaya, Ursula von der Leyen, alisema Jumatano kwamba Umoja wa Ulaya (EU) unapanga kugawanya msaada wa kifedha wa…

Rais wa Tume ya Ulaya, Ursula von der Leyen, alisema Jumatano kwamba Umoja wa Ulaya (EU) unapanga kugawanya msaada wa kifedha wa euro bilioni 90 uliokubaliwa kuisaidia Ukraine.

Kulingana na mpango huo, theluthi moja ya fedha hizo sawa na euro bilioni 30 itatumika kusaidia bajeti ya kawaida ya serikali ya Ukraine, huku theluthi mbili zilizobaki euro bilioni 60 zitaelekezwa katika ununuzi wa vifaa vya kijeshi.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari mjini Brussels, von der Leyen alisema hatua hiyo inalenga kuimarisha msaada wa EU ili kujenga Ukraine iliyo imara na yenye uthabiti zaidi.

Aliongeza kuwa fedha za euro bilioni 60 zitakazotumika kwa ajili ya vifaa vya kijeshi zitatumika hasa kununua silaha na vifaa vingine kutoka nchi wanachama wa EU na zile za EFTA (Jumuiya ya Biashara Huria ya Ulaya)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *