Operesheni ya kutafuta miili ya watu waliofariki inaendelea mashariki mwa DRC kufuatia kuporomoka kwa udongo kwenye mgodi wa koltani huko Rubaya, Kivu Kaskazini, Jumanne, Machi 3, eneo linalodhibitiwa na kundi lenye silaha la AFC/M23.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Idadi ya vifo bado haijulikani, lakini kulingana na vyanzo kadhaa, shughuli za uchimbaji madini zimesimamishwa na zoezi la kutafuta miili linaendelea. Mwishoni mwa mwezi Januari, maporomoko makubwa ya ardhi katika eneo hilo yalisababisha vifo vya wachimbaji zaidi ya 200.

Maporomoko haya ya hivi karibuni, yaliotokea Machi 3, katika mgodi wa koltani baada ya maporomoko ya udongo katika eneo la uchimbaji madini la Gasasa, karibu na Rubaya, huko Kivu Kaskazini. Idadi ya vifo bado haijabainika, lakini mashirika ya kiraia yana wasiwasi. Mwishoni mwa mwezi Januari, maporomoko makubwa ya ardhi katika eneo hilo la uchimbaji madini yaliwaua zaidi ya watu 200, kulingana na vyanzo vya ndani na serikali.

Huu ni mgodi unaochimbwa kienyeji ambapo mamia ya wachimbaji wadogo mara nyingi hufanya kazi bila ulinzi wowote na katika ardhi isiyo imara, wakiwa wamedhoofishwa na miaka kadhaa ya uchimbaji. Akihojiwa na RFI, Jean-Pierre Okenda, mkurugenzi wa Shirika Lisilo la Kiserikali la Kongo la La Sentinelle des ressources naturelles (Mlinzi wa Maliasili), ameelezea sababu za kuanguka huku mfululizo:

” Kumekuwa na maporomoko ya ardhi mara kwa mara kwa sababu mashimo huchimbwa kwa mikono, hayajengeki vizuri, na hayafanyiwi matengenezo.”

“Watu huchimba kila mahali, bila udhibiti au hatua za usalama. Katika shimo moja wanaweza kuwepo wachimbaji hadi 500, na kwa kuwa vishimo vinakwenda sambamba, shimo moja likiporomoka linaweza kuathiri mengine mengi kwa wakati mmoja,” Jean-Pierre Okenda ameongeza.

Nchini DRC, kanuni za uchimbaji madini hupunguza kina cha juu cha usaidizi hadi mita 30. Kwa bahati mbaya, wachimbaji wanaotumia mfumo wa kienyeji huchimba zaidi ya kina hiki kwa sababu wanafuata njia ya madini. Na wakati mwingine huenda zaidi ya mita 60… na ikiwa hilo litatokea katika hali ambapo, kwa mfano, kuna mvua kubwa, basi, katika hatua hiyo, kwa kawaida kuna kuanguka kwa kuta za shimo.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *