Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema operesheni za jeshi la nchi yake nchini Iran zitamalizika karibuni, akitoa hakikisho kwa masoko ya dunia ambayo yametetereka kutokana na mzozo unaoendelea mashariki ya kati.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Kauli ya Trump, anaitoa wakati ambapo jeshi lenye nguvu nchini Iran likidai lenyewe ndilo litakaloamua vita iishe lini, wakati huu pia likiapa kuwa tiifu kwa kiongozi mpya wa juu wa kidini, Mojtaba Khamenei.
Masoko ya dunia yalikuwa yameporomoka kutokana na vita vya Mashariki ya kati, bei za mafuta zikionekana kupanda Jumatatu ya wiki hii.
Tehran chini ya uongozi wa kiongozi wake mpya Mojtaba Khamenei, imeendelea kurusha makombora kuelekea majirani zake katika nchi za Ghuba, ikiaashiria kwamba mfereji wa Hormuz huenda ukaendelea kufungwa.
Licha ya Rais Trump kudai kwamba vita hivyo vinakaribia kumalizika, jeshi la mapinduzi la Iran limetupilia mbali kauli yake kuhusu vita hivyo likisema kwamba ndilo litakaloamua ni lini vita vitamalizika.
Tangazo la Trump limejiri wakati huu wanajeshi wa Iran wakiripotiwa kuanzisha mashambulio mapya ya makombora na droni katika nchi za Saudi Arabia, Bahrain, Qatar,UAE na Israel.
