Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky anatarajiwa nchini Uhispania “katika siku zijazo,” Waziri wa Ulinzi wa Uhispania Margarita Robles ametangaza Jumatano, bila kutaja tarehe ya ziara hiyo.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

“Hatuwezi kusahau Ukraine… Rais Zelensky atakuja katika siku zijazo,” amesema Waziri wa Ulinzi wa Uhispania Margarita Robles katika mkutano na waandishi wa habari mnamo Machi 11. 

Waziri huyo hakutoa maelezo zaidi kuhusu ziara ya Volodymyr Zelensky, ambayo itakuwa ya nne nchini Uhispania tangu kuanza kwa mashambulizi makubwa ya Urusi nchini Ukraine mnamo Februari 2022, kulingana na shirika la habari la AFP.

Spika wa Bundestag asisitiza uungaji mkono wa Ujerumani kwa Ukraine

Spika wa Bunge la Ujerumani (Bundestag), yuko Kyiv leo Jumatano kuthibitisha uungaji mkono wa Berlin wakati ambapo vita vya Mashariki ya Kati vinapotosha umakini wa jumuiya ya kimataifa kutoka kwa vita vya Urusi nchini Ukraine.

Julia Klöckner, mwenye umri wa miaka 53, amepangwa kukutana na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky baada ya hotuba katika bunge la Ukraine, Bundestag imetangaza katika taarifa. Ni mwakilishi wa kwanza wa Ujerumani kuhutubia bunge, kulingana na chanzo hicho

“Hasa sasa, kwa kuzingatia sana hali ya Mashariki ya Kati, hatupaswi kupoteza mtazamo wa vita vya uchokozi vya Urusi dhidi ya Ukraine,” Julia Klöckner amesema, akinukuliwa katika taarifa hiyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *