
Tukio la kushangaza lilitokea kati ya wajumbe wa Rwanda na Kongo siku Jumanne, Machi 24, katika hoteli huko Washington, D.C., ambapo Mke wa rais wa Kongo, Denise Nyakeru Tshisekedi, alifikia. Uvumi wa “jaribio la mauaji” ulienea haraka mtandaoni nchini DRC. Ubalozi wa Rwanda nchini Marekani unakanusha madai haya.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Katika video inayosambaa mtandaoni, wanaume waliovaa miwani yenye rangi wanaonekana wakipakia masanduku kwenye gari la ubalozi kabla ya kuondoka hotelini huko Washington, D.C. ambapo Denise Nyakeru Tshisekedi alikuwa akiishi. Kwa mwaliko wa mke wa Rais Donald Trump, mke wa Félix Tshisekedi alitarajiwa kuhudhuria mkutano wa kilele na wake wengine wa rmarais.
Mamlaka ya nchi zote mbili zilijibu haraka. Msemaji wa serikali ya Kongo Patrick Muyaya alithibitisha jaribio la kujipenyeza kwa raia wa Rwanda, akiongeza kuwa Mke wa rais Tshisekedi “anaendelea vizuri.” Serikali ya Kongo inasema inawasiliana na mamlaka ya Marekani ili kufafanua mazingira ya tukio hilo.
“Tukio limetatuliwa bila machafuko,” kulingana na ubalozi wa Rwanda
Katika taarifa iliyotolewa Jumanne usiku, ubalozi wa Rwanda nchini Marekani ulishutumu “matukio yaliyopotoshwa vibaya” na kutoa toleo tofauti la matukio. Kulingana na ujumbe wa ubalozi wa Rwanda, afisa wa usalama wa mmoja wa viongozi wa Rwanda ambaye hakuwa na silaha “alikutana kwa bahati mbaya na maafisa wa usalama” wa ujumbe wa Kongo katika hoteli ambayo makundi hayo mawili yalikuwa yamefikia.
Maafisa wa Kongo kisha wanaripotiwa “kuzuia kwa muda ufikiaji wa lifti.” Ubalozi wa Rwanda ulielezea tabia hiyo kama “isiyofaa na isiyokubalika,” ingawa “tukio hilo hatimaye lilitatuliwa bila vurugu,” taarifa hiyo iliongeza.
Rwanda, ambayo inadai kwamba ujumbe wake “ulinyanyaswa na kurekodiwa na watu wasiojulikana ulipokuwa ukiondoka,” pia ililaani “uongo uliyojaa kejeli” kutoka mamlaka ya Kongo, “ambao unapazwa kupuuzwa na kulaaniwa.”