Rais wa Marekani Donald Trump amefuta picha aliyokuwa ameichapisha katika mtandao wake wa kijamii inayomfananisha na Yesu baada ya viongozi wa kidini kumkosoa vikali na kuitaja dhihaka na kukufuru.

Rais Trump anasema alidhani Picha hiyo aliyotengeza kwa kutumia akili mnemba inamuonesha kama Daktari na sio Yesu.

Hayo yanakuja baada ya Kiongozi huyo wa Marekani kujibizana vikali na Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Leo kuhusu vita vya Mashariki ya Kati.

Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance amesema Makao makuu ya Kanisa Katoliki Vatican yanapaswa kujikita katika masuala ya kimaadili na kumuacha Rais Trump kujikita katika masuala ya Sera za Kisiasa.

(Feed generated with FetchRSS)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *