
Jeshi la Israel limeendelea kuttekeleza mashambulizi katika maeneo mbalimbali ya Lebanon saa chache baada ya usitishaji mapigano kati ya Lebanon na Israel kuanza kutekelezwa.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Na mwandishi wetu huko Beirut, Paul Khalifeh
Kwa kweli kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa viwango tofauti katika saa za hivi karibuni, lakini katika hatua hii, hatuwezi kuzungumzia kuvunjika kwa usitishaji mapigano. Mapigano, wakati mwingine ya vurugu, yanayohusisha silaha za kivita na roketi, yanatokea mara kwa mara katika jiji la Bint Jbeil, katika eneo la kati la kusini mwa Lebanon, na katika mji mkubwa wa mpakani wa Khiyam, mashariki mwa Lebanon.
Vifaru vya Israel vilirusha makombora takriban kumi katika kijiji kimoja, na Hezbollah ilidai kuhusika na kurusha roketi nyingi dhidi ya kundi la wanajeshi wa Israel katika eneo la mashariki la kusini mwa Lebanon. Ndege isiyo na rubani ya Israel pia ilishambulia gari moja katika eneo lililo umbali wa kilomita kumi kutoka mpakani.
Licha ya ukiukaji huu, kiwango cha vurugu hakiwezi kulinganishwa na ukubwa wa mapigano yaliyorekodiwa kabla ya kuanza kwa makubaliano ya kusitisha mapigano. Siku ya Alhamisi pekee, jeshi la anga la Israel lilifanya mashambulizi zaidi ya 380 katika maeneo mbalimbali ya Lebanon, na Hezbollah ilirusha mamia ya roketi na kurusha ndege zisizo na rubani kadhaa dhidi ya jeshi la Israel kusini mwa Lebanon na kaskazini mwa Galilaya.
Hakujakuwa na uhakika kuhusu kurudi kwa watu waliokimbia makazi yao ikilinganishwa na wale waliorekodiwa wakati wa vita vya awali na Israel. Jeshi la Lebanon, Hezbollah, na Spika wa Bunge, Nabih Berri, mwenyewe kutoka kusini mwa Lebanon, wametoa wito kwa watu waliokimbia makazi yao wasirudi vijijini mwao kutokana na hatari inayoendelea.
Licha ya wito huu, mamia ya magari yameelekea vijijini kusini mwa Mto Litani. Msongamano wa magari umeripotiwa karibu na madaraja yanayozunguka mto, ambayo yalikuwa yameharibiwa na mashambulizi ya anga ya Israel. Watu wengi wameonekana wakirudi kusini mwa Beirut, ambapo watu 700,000 walitoroka mji huo.