Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, mapokezi ya wahamiaji waliofukuzwa nchini Marekani yanaibua maswali mengi. Kundi la kwanza la wahamiaji kumi na watano kutoka Peru, Colombia, na Ecuador waliwasili Kinshasa siku ya Ijumaa, Aprili 17, kama sehemu ya makubaliano yaliyofikiwa na utawala wa Marekani. 

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu huko Kinshasa, Pascal Mulegwa

Uhamisho zaidi unaweza kufuata katika siku zijazo, wakati utata tayari unaongezeka. Kwa mashirika ya kiraia, ukosefu wa uwazi unaozunguka hali ya wahamiaji hawa unaweza kuwa ukiukaji wa haki zao za msingi. Mashirika ya kiraia yanalaani kutoonekana uwazi wa kesi hiyo, huku upinzani ukipaza sauti na unaendelea kutiliwa shaka.

Chama kikubwa zaidi cha upinzani katika Bunge la DRC kinashikilia msimamo wake na kinataka uwazi zaidi, kama ilivyobainishwa na Olivier Kamitatu, msemaji wa Moïse Katumbi, kiongozi wa chama cha Ensemble pour la République. “Tunadai kuchapishwa kwa makubaliano haya kwa sababu tuna sababu kubwa za kuamini kwamba makubaliano haya sio siri. Raia wa Kongo wana haki ya kujua kile kilichosainiwa kwa niaba lao.” Serikali ambayo haiwezi kudhibiti mipaka yake ya mashariki, ambayo haiwezi kuwalinda raia wake, ghafla itaweza kusimamia vituo vya kuwashikilia raia wa kigeni wenye wasifu unaotiliwa shaka, kwa watu wasiojulikana. Hiyo iinakuwa hadithi ya kubuni.”

Kwa upande wa upinzani, kubadilika kwa utawala wa Tshisekedi kuelekea utawala wa Trump kimsingi kunaficha ajenda ya kisiasa, anaelezea Olivier Kamitatu. “Félix Tshisekedi anatafuta ulinzi wa Washington kwa muhula wa tatu, jambo ambalo Katiba inapinga. Kwa hivyo yuko tayari kuweka rehani heshima ya Kongo kwa ajili ya kuendelea kusalia malakani. Kongo haiuzwi kabisa.”

Serikali yakanusha shutma za upinzani

Shtuma hizi zimefutlia mbali kabisa na Jean Thierry Monsenempwo, msemaji wa muungano tawala, Muungano Mtakatifu. “Mambo yote hayapaswi kuingizwa kisiasa.” Hebu tuangalie ukweli. Makubaliano haya ni mbinu ya kimkakati. yanaimarisha uhusiano na nguvu inayoongoza duniani na kufungua matarajio ya ushirikiano wa usalama wa kiuchumi na ushawishi wa kimataifa. Kinshasa inaendelea kuwa na haki ya uhuru wa kusitisha makubaliano hayokwa  wakati wowote. Kile ambacho DRC inafanya ni utaratibu wa kawaida wa kidiplomasia. Mkataba huu unaambatana na moyo wa Mkataba wa Kimataifa wa Uhamiaji Salama, Utaratibu, na wa Kawaida. Marekani haiwahamishi wafungwa, bali watu walio katika hali ya uhamiaji ambao wanahitaji kushughulikiwa.

Muda wa kukaa kwa wahamiaji hawa, waliohifadhiwa katika hoteli iliyo nje kidogo ya Kinshasa, haujulikani. Pia kuna swali la hali yao na uhuru wao wa kutembea ndani ya mji mkuu wa Kongo. Lakini katika hatua hii, serikali haijatoa majibu yoyote kwa maswali yoyote haya.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *