
Nchini Chad karibia watu 42 wameuwawa baada ya makabiliano na mapigano kuzuka Jumapili kati ya makabila yanayoishi mashariki mwa nchi hiyo.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Kwa mujibu wa ripoti ya Mjumbe wa serikali aliyefika eneo hilo mapigano hayo yalianza kufuatia mzozo wa kisima kimoja katika kijiji kidogo cha Guereda kilichoko jimbo la Wadi Fira Mashariki mwa nchi hiyo.
Kufuatia hali hiyo mbaya ya kiusalama, Mawaziri kadhaa, maafisa wakuu wa eneo hilo, na mkuu wa majeshi walitumwa kwenye eneo la tukio kutathmini hali ilivyo.
Limane Mahamat Naibu Waziri Mkuu anayesimamia Utawala wa wilaya na ugatuzi, kwenye taarifa yake kwa kituo cha utangazaji cha serikali alisema, hali hiyo imedhibitiwa kwa sasa na utumivu umerejea
Kwa miaka kadhaa, eneo la mashariki mwa Chad limekuwa likikumbwa na migogoro kati ya wakulima na wafugaji wa Kiarabu. Mvutano huo ukizidishwa na wakimbizi wanaokimbia mapigano katika nchi jirani ya Sudan.
Migogoro hiyo kuhusu mashamba na malisho ya mifugo imesababisha vifo vya zaidi ya elfu moja na wengine 2,000 kujeruhiwa kati ya mwaka wa 2021 na mwaka wa 2024, kulingana na ripoti ya Shirika lisilo la Kiserikali la International Crisis Group.