Chanzo cha picha, Getty Images
Muda wa kusoma: Dakika 2
Newcastle imeingia katika kinyang’anyiro cha kumsajili mshambuliaji wa Senegal Nicolas Jackson, 24, anayetarajiwa kurejea Chelsea mwishoni mwa msimu baada ya Bayern Munich kuthibitisha kuwa haitageuza mkopo wake kuwa uhamisho wa kudumu.
Nottingham Forest inamfikiria kiungo wa Middlesbrough Hayden Hackney, 23, kama mbadala wa Elliot Anderson iwapo ataondoka majira ya kiangazi. Haya ni kwa mujibu wa (Talksport)
Atletico Madrid inatarajiwa kuingia katika ushindani na Tottenham kwa ajili ya beki wa Scotland Andy Robertson, 32, ambaye amesema ataondoka Liverpool mkataba wake utakapomalizika mwezi Juni.Haya ni kwa mujibu wa Sun
Chelsea inamfikiria kocha wa Napoli Antonio Conte kama mmoja wa wanaoweza kuchukua nafasi ya Liam Rosenior kwa kudumu msimu ujao.Express)
Kocha wa Porto Francesco Farioli pia yuko kwenye orodha ya Chelsea, ingawa mkataba wake unaendelea hadi 2028 na una kipengele cha kuvunja mkataba cha euro milioni 20. (Nicolo Schira)
Arsenal na Chelsea ni miongoni mwa klabu za Ligi Kuu England zilizomfuatilia mshambuliaji wa Ubelgiji Mika Godts, 20, baada ya kufunga bao la kuvutia akiwa na Ajax mwishoni mwa wiki.
Manchester United inafuatilia hali ya Xavi Simons huko Tottenham huku ikitathmini uwezekano wa kumsajili kiungo huyo wa Uholanzi, 23, katika dirisha la majira ya kiangazi.(Fichajes – in Spanish)
Everton inamuwania kiungo wa Aston Villa na Scotland John McGinn, 31. (Football Insider)Liverpool inajiandaa kwa ushindani wa kumbakisha kipa wa Brazil Alisson Becker, 33, huku Juventus ikionyesha nia ya kumsajili.
Kiungo wa Manchester City Bernardo Silva, 31, anawaniwa na Juventus, Barcelona, Paris Saint-Germain na Al Hilal.
Beki wa England John Stones, 31, amejiweka katika rada za Barcelona huku akielekea mwisho wa maisha yake Manchester City.
Liverpool imeanzisha mawasiliano na wawakilishi wa winga wa RB Leipzig Yan Diomande, 19, kutoka Ivory Coast. (Football Insider)