
Jeshi la Israel limetangaza leo Ijumaa kuwa mwanajeshi wa Israel ameuawa kusini mwa Lebanon, na kufanya idadi ya vifo kufikia 20 katika mapigano na Hezbollah inayounga mkono Iran tangu mapema mwezi Machi.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Sajenti Meja Negev Dagan, 20, “almeuawa vitani kusini mwa Lebanon,” jeshi la Israel limesema katika taarifa.
Kwa jumla, wanajeshi 20 wa Israel wameuawa nchini Lebanon—wanajeshi 19 na mkandarasi mmoja anayefanya kazi kwa jeshi—tangu kuanza kwa vita mnamo Machi 2. Katika kipindi hicho, mashambulizi ya anga ya Israel yaliwaua zaidi ya watu 2,800 nchini Lebanon, wakiwemo watoto wasiopungua 200, kulingana na Beirut.
Hezbollah inasema iliwalenga wanajeshi nchini Israel
Hezbollah imesema kwamba ilitumia ndege isiyo na rubani kushambulia wanajeshi wa Israel kaskazini mwa Israel, karibu na mpaka na Lebanon. Jeshi la Israel hapo awali liliripoti kwamba shambulio la ndege isiyo na rubani ya Hezbollah liliwajeruhi raia kadhaa, ambao walipelekwa hospitalini.
Jeshi la Israel pia lilitangaza wimbi jipya la mashambulizi dhidi ya Hezbollah nchini Lebanon na kuwata raia kuhama vijiji zaidi ya kumi kusini mwa nchi hiyo.