r

Chanzo cha picha, Reuters

Rais wa Marekani Donald Trump amesema mazungumzo ya biashara kati ya Marekani na China “yamekwenda vizuri zaidi kuliko mara ya mwisho”, akieleza kuwa safari hii yalikuwa makubwa zaidi kuliko makubaliano 36 yaliyosainiwa katika mazungumzo yaliyopita.

Trump amesema China itanunua kiasi kikubwa cha mazao ya kilimo kutoka Marekani, ikiwemo maharage ya soya.

Alipoulizwa na mtangazaji wa Fox News Sean Hannity kuhusu kile ambacho China inataka kutoka Marekani, Trump alijibu: “Ni mambo mengi sana ya kujadili, lakini yapo mengi,” bila kutoa maelezo zaidi.

Katika mazungumzo hayo, Trump pia amesema China imekubali kununua mafuta kutoka Marekani.

“Tutaona meli za China zikielekea Texas, Louisiana na Alaska,” anasema, akiongeza kuwa nishati ndiyo bidhaa ambayo China inaihitaji zaidi.

“Tunayo nishati isiyo na kikomo,” alisema.

Trump pia amedai kuwa Rais wa China Xi Jinping amekubali kununua ndege 200 za kampuni ya Boeing, akieleza hatua hiyo kama “ahadi kubwa”.

“Ndege 200 kubwa, hiyo ni ajira nyingi. Boeing walitaka 150, lakini wamepata 200,” alisema.

Mapema, Waziri wa Hazina wa Marekani alikuwa amedokeza uwezekano wa China kutangaza oda kubwa ya ndege za Boeing, akiiambia CNBC kuwa Beijing huenda ikatangaza rasmi ununuzi huo hivi karibuni.

Trump amehitimisha kwa kusema amefanikisha zaidi kuliko viongozi wengine katika kushughulikia biashara na China, akidai nakisi ya biashara kati ya nchi hizo imepungua kwa kiwango kikubwa ikilinganishwa na ilivyokuwa awali.

Trump na wafanyibiashara alioandamana nao China watakamilisha ziara yao hii leo.

Soma zaidi:

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *