Mexico: Kumi waangamia katika shambulio la watu wenye silaha katika jimbo la PueblaMexico: Kumi waangamia katika shambulio la watu wenye silaha katika jimbo la Puebla

Mamlaka ya Mexico imetangaza siku ya Jumapili kwamba angalau watu kumi waliuawa katika shambulio la watu wenye silaha katika jiji la Tehuitzingo, katika jimbo la mashariki mwa kati la Puebla.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Na: RFI na mashirika mengine

Matangazo ya kibiashara

Wanaume sita, wanawake watatu, na mtoto mmoja walikuwa waathiriwa shambulio jana usiku, idara ya usalama wa umma ya Puebla ilisema katika taarifa. Mamlaka ya shirikisho inafanya uchunguzi.

Mamlaka katika eneo hilo hazikubainisha kama kulikuwa na washukiwa wowote katika mauaji hayo.

Mnamo mwezi Februari, watu sita waliuawa huko Huehuetlán El Grande, jiji lingine katika jimbo la Puebla. Siku chache baadaye, watu watatu waliuawa katika mji mkuu wa Puebla baada ya shambulio kwenye gari lao.

Gavana wa Puebla Alejandro Armenta bado hajazungumza chochote kuhusu matukio ya Jumapili.

Hivi majuzi eneo la katikati ya Mexico lilishuhudia ongezeko la vurugu zinazohusiana na kundi la kigaidi, na kusababisha kati ya familia 800 na 1,000 kutoroka makazi yao.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *