Kenya: Wanne wamefariki katika maandamano dhidi ya ongezeko la bei ya mafutaKenya: Wanne wamefariki katika maandamano dhidi ya ongezeko la bei ya mafuta

Nchini Kenya, watu wanne wameuawa na zaidi ya thelathini kujeruhiwa siku ya Jumatatu, Mei 18, wakati wa vurugu zilizoshuhudiwa siku ya mgomo wa usafiri wa umma na maandamano ya kupinga ongezeko la bei ya mafuta hivi karibuni. Hili lilitangazwa mapema Jumatatu jioni na Waziri wa Mambo ya Ndani. Kwa sasa, serikali ya Kenya haijatoa maelezo zaidi kuhusu eneo au mazingira ya matukio haya, lakini imewanyooshea kidole wale wanaochochea vurugu nchini.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

“Tutaimarisha mapambano yetu dhidi ya uhalifu uliopangwa na wale ambao wameazimia kueneza machafuko,” Waziri wa Mambo ya Ndani Kipchumba Murkomen alisema katika taarifa.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Kenya iliorodhesha matukio mbalimbali yaliyotokea nchini Jumatatu, ikiwa ni pamoja na uporaji wa maduka makubwa kadhaa, kuchomwa moto kwa ofisi ya UDA (chama tawala) katika Kaunti ya Makuena, kusini mwa mji mkuu, Nairobi, na uharibifu wa malori mawili kwenye barabara ya Rironi-Mau Summit.

Ingawa taarifa hiyo haikueleweka kuhusu sababu za mashambulizi haya na mazingira ya kuongezeka kwa vurugu zilizosababisha vifo vya watu wanne, Wizara ya Mambo ya Ndani inabaini kwamba “baadhi ya wanasiasa wanatoa matamshi ya uchochezi ili matamshi ya uchochezi ili kuhimiza kutovumiliana, ukabila, na kwamba magenge yanajipanga kueneza ugaidi.”

Kama ukumbusho, mgomo huo ulizinduliwa na muungano wa wadau wa sekta ya uchukuzi ambao waliapa kuzuia shughuli zote kufuatia ongezeko zaidi la bei za mafuta kwenye vituo vya mafuta mnamo Mei 14, hatua iliyochukuliwa na serikali.

Barabara zilizofungwa zinasafishwa kuanzia Jumatatu jioni, kulingana na Wizara ya Mambo ya Ndani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *