“Mtesaji maarufu,” mkurugenzi wa zamani wa gereza la Libya anakabiliwa na mashtaka ya ICC“Mtesaji maarufu,” mkurugenzi wa zamani wa gereza la Libya anakabiliwa na mashtaka ya ICC

Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu imefungua vikao vya mashtaka kwa Khaled Mohamed Ali el-Hishri, mmoja wa makamanda wa gereza la Mitiga nchini Libya. El-Hishri anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita, ikiwa ni pamoja na ubakaji, unyanyasaji wa kijinsia, mateso, na dhulma nyingine mbalimbali. Kwa siku tatu, mwendesha mashtaka atajaribu kuwashawishi majaji kuthibitisha mashtaka na kumpeleka mahakamani. Kisha watakuwa na siku 60 kufikia uamuzi.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu huko Hague, Stéphanie Maupas

“Malaika wa Kifo” ni jina lililotolewa na baadhi ya mashahidi katika kesi ya upande wa mashtaka… Khalid el-Hishri alikuwa “mtesaji maarufu,” alisema Naibu Mwendesha Mashtaka Nazhat Khan.

Siku ya kwanza ya kusikilizwa kwa kesi hiyo iliiingiza mahakama katika ulimwengu wa kutisha wa gereza la Mitiga, ambapo, kulingana na upande wa mashtaka, mfumo wa mateso ulioanzishwa ulikuwapo. Upande wa mashtaka ulielezea hali ya kizuizini huko Mitiga, ambapo maelfu ya wafungwa, kwa sehemu kubwa, walikuwa raia, pamoja na wapiganaji wachache wasio na silaha. Wafungwa wote walihojiwa na kuteswa, wakilala katika vyumba vilivyojaa watu bila chakula cha kutosha, bila huduma ya matibabu, na bila dawa.

“Khalid el-Hishri alifanya makosa na hajaadhibiwa kabisa”

Mbele ya majaji watatu, naibu mwendesha mashtaka alielezea muktadha wa uhalifu anaomshutumu mwanamgambo Khalid El Ishri : “Khalid el-Hishri alitekeleza uhalifu wake bial kujali na hajaadhibiwa kabisa hadi alipokamatwa mwaka jana. Yeye na viongozi wengine wa Vikosi Maalum, vinavyodhibiti eneo la gereza la Mitiga, walitenda uhalifu bila matokeo au mipaka yoyote, kutokana na ukosefu wa usalama uliojitokeza baada ya kuanguka kwa utawala wa Gaddafi na kwa sababu ya mgogoro unaoendelea, ambao unawaruhusu kukusanya nguvu na rasilimali nyingi.”

Inadaiwa Khalid el-Hishri hakuamuru tu uhalifu huo kwa walinzi, au kwa baadhi ya wafungwa walioshiriki, lakini pia alishiriki kibinafsi. Kulingana na upande wa mashtaka, yeye mwenyewe alibaka, kutesa, na kuwaua wafungwa kadhaa. Walianza kuelezea kwa undani utendaji kazi wa wanamgambo, Kikosi Maalum, ambacho wakati fulani kilihudumiwa na serikali ya Tripoli kupambana na ugaidi na uhalifu uliopangwa.

Vikao hivyo vitaendelea hadi Alhamisi, Mei 21, huku mawakili wa waathiriwa na upande wa utetezi wakisikilizwa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *