Serikali ya Afrika Kusini inasema, inashughulikia suala la kuwepo kwa raia wa kigeni wanaoishi nchini humo bila vibali, ikiwataka raia wa nchi hiyo kutochukua hatua mikononi mwao.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Kauli hii ya serikali inakuja wakati huu maandamano dhidi ya wageni wanaoishi nchini humo bila vibali, yakiendelea kwenye miji mbalimbali.
Mawaziri mbalimbali wamekutana kwenye kikao cha dharura kujadili madai kuwa wageni wasio na vibali, wanasababisha visa vya utovu wa usalama nchini humo na kuchukua ajira za wenyeji.
Naibu Waziri wa Mambo ya ndani Njabulo Nzuza amesema, Afrika Kusini inakabiliwa na changamoto kubwa ya wahamiaji haramu na inataka mchakato wa kuwaondoa nchini humo ufuate sheria.
Hii inakuja baada ya wiki iliyopita, mamia ya raia wa kigeni kutoka mataifa kama DRC, Rwanda na Somalia kutafuta hifadhi kwenye mji wa Durban baada ya kupokea vitisho kutoka kwa wenyeji kuwa, kufikia Juni tarehe 30 wawe wameondoka nchini humo.
