Uswisi yakosolewa kwa kuwarudisha kwa nguvu nyumbani waomba hifadhi kutoka BurundiUswisi yakosolewa kwa kuwarudisha kwa nguvu nyumbani waomba hifadhi kutoka Burundi

Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa na mashirika 40 yasiyo ya kiserikali yanaikosoa Uswisi kwa kuwarudisha kwa nguvu nyumbani waomba hifadhi kutoka Burundi.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Uswisi ni mojawapo ya nchi chache za Ulaya kutekeleza mpango wa kurudisha kwa nguvu nyumbani waomba hifadhi katika nchi inazoona kuwa salama. Hata hivyo, katika kesi ya Burundi, inategemea uamuzi wake juu ya tathmini iliyopitwa na wakati, wakati nchi hiyo inashtumiwa kwa kuwanyanyasa raia, hasa wafuasi na viongozi wa upinzani, kulingana na mashirika ya haki za binadamu. Raia kumi na mmoja kutoka Burundi, ikiwa ni pamoja na familia moja yenye watoto, walirudishwa nyumbani mwezi uliopita.

Eric (sio jina lake halisi) alikimbia Burundi baada ya kuteswa gerezani kwa kupinga  wanamgambo wa Imbonerakure, vijana kutoka chama tawala cha CNDD-FDD. “Nilifungwa kwa wiki tatu katika moja ya magereza ya Idara ya ujasusi. Niliteswa kimwili na nilifanyiwa unyanyasaji wa kijinsia wa kutisha,” anasema.

Akiwa mkimbizi nchini Uswisi tangu mwaka 2022, ambapo ombi lake la hifadhi lilikataliwa, Eric anaweza kufukuzwa wakati wowote.

“Tangu siku hiyo, nimekuwa nikiishi katika hali ya dharura. Siwezi kulala vizuri, natumia dawa za msongo wa mawazo,” anaongeza. “Ninapofikiria kurudishwa Burundi baada ya yote niliyopitia, ni vigumu sana kwangu.”

Kutoroka nchi ni kitendo cha kutokuwa na imani na utawala wa Burundi

Emma Lidén ni wakili wa haki za binadamu huko Geneva. Aliwasilisha kesi ya Eric kwa Mwandishi Maalum wa Umoja wa Mataifa. “Mamlaka Uhamiaji itatathmini upya uamuzi wake kufuatia hali ya haki za binadamu nchini Burundi. Mamlaka zinahitajika kutathmini kila hali kibinafsi na kwa njia ya kisasa,” anaeleza.

Mamlaka ya Uswizi hutathmini hatari za usalama na kutoa hadhi ya ukimbizi kulingana na wasifu wa mwanaharakati wa waomba hifadhi. Mwandishi Maalum wa Umoja wa Mataifa anabainisha katika ripoti yake kwamba kutoroka tu nchi ni kitendo cha kutokuwa na imani na utawala wa Burundi, na kufanya wakimbizi hao kurudi nyumbani kuwa hatari zaidi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *