Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) anatarajia kuondoka Kinshasa leo Jumatatu jioni, Juni 1, baada ya mkutano na Rais Félix Tshisekedi. Tedros Ghebreyesus anahitimisha ziara ya siku nyingi nchini humo, ambapo alizuru Bunia, mji ambao kwa sasa ni kitovu cha mlipuko wa virusi vya Ebola. 

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu huko Kinshasa, Paulina Zidi

Sehemu ya majibu ya kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huo imejikita katika mji huo. Huko Bunia, alikutana na ujumbe wa mawaziri, wakiwemo Mawaziri wa Afya na Mawasiliano wa Kongo. Waatatu hao walionysha mshikamano wao dhidi ya ugonjwa huo hatari.

Viongozi hao watatu walifanya mkutano na waandishi wa habari mwishoni mwa Jumamosi, Aprili 30, na kisha wakatoa taarifa waliporejea kutoka Bunia Jumapili jioni. Msimamo wa umoja ambao haukuonekana wakati Tedros Ghebreyesus alipowasili nchini.

Huko Kinshasa, baadhi ya maafisa wametilia shaka mawasiliano ya WHO, ambayo wakati mwingine waliyaelezea kama “mabaya.” Mamlaka inatia mbele uzoefu wa nchi hiyo, baada ya kukabiliwa na mlipuko wa 17 wa Ebola, katika jaribio la kuhakikishia umma. Lakini huko Bunia, “tulikuwa na majadiliano ya wazi ambayo yalituwezesha kusonga mbele,” amekiri mjumbe afisa kutoka ujumbe wa mawaziri.

Habari za kutia moyo

Tangu wakati huo, habari za kutia moyo pia zimesaidia kupunguza mvutano: kama vile kupona kwa wagonjwa kadhaa na kufunguliwa kwa kituo cha matibabu ya Ebola huko Bunia, kituo ambacho kilifunguliwa na Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka siku ya Jumapili. Na jumbe zilizorudiwa na WHO zinazohimiza kuondolewa kwa vikwazo vya usafiri, zimepokelewa vyema huko Kinshasa.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani anatarajiwa kurejelea ujumbe wake wa usaidizi kwa watu walioathiriwa lakini pia imani yake kwa mamlaka. Pia atahutubia jumuiya ya kimataifa, akitoa wito wa mshikamano na uwezo zaidi wa kifedha na vifaa. “Kumekuwa na ahadi, lakini zinahitaji kutimizwa,” chanzo cha WHO kimesema.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *