Chanzo cha picha, Getty Images
Hispania ilistahili kushinda fainali ya Kombe la Dunia baada ya ushindi mwembamba dhidi ya Argentina iliyobaki na wachezaji 10, huku bao la Ferran Torres katika muda wa nyongeza likivunja upinzani wao.
Mabingwa wa Ulaya walitengeneza nafasi bora zaidi dhidi ya mabingwa watetezi wa dunia, ambao kwa kiasi kikubwa walitegemea mbinu za kuchelewesha mchezo na kuharibu kasi ya wapinzzani.
Enzo Fernandez alitolewa kwa kadi nyekundu muda mfupi kabla ya mchezo kuingia katika muda wa nyongeza.
Torres alikuwa shujaa wa Hispania alipoupokea mpira wa kichwa kutoka kwa mchezaji aliyeingia akitokea benchi, Nico Williams, na kumshinda mlinda lango wa Argentina Emiliano Martinez kwa shuti kali la karibu katika dakika ya 106.
Mchezo huo uligeuka kuwa pambano la nguvu na tahadhari badala ya soka la kuvutia. Wakati huo huo, mbali na uwanja, fainali hiyo ilikuwa ya kipekee kwa shamrashamra na uwepo wa mastaa mbalimbali.
Rais Donald Trump aliwasili New Jersey kwa msafara wa helikopta kabla ya mchezo kuanza, huku Shakira, Madonna na Justin Bieber wakitumbuiza katika onesho la kwanza kabisa la mapumziko ya kipindi cha kwanza katika historia ya Kombe la Dunia, na kufanya mapumziko hayo yadumu kwa dakika 27.
Katika mchezo uliokuwa na makosa mengi na kusimamishwa mara kwa mara, Hispania ilionekana kuwa bora zaidi, huku Lamine Yamal na Mikel Oyarzabal wakimlazimisha Emiliano Martinez kuokoa mipira muhimu katika kipindi cha kwanza.
Wachezaji wa Hispania walimlalamikia mara kwa mara mwamuzi Slavko Vincic kwa kuwa mpole katika kutoa adhabu, hasa baada ya Alexis Mac Allister kumchezea vibaya Dani Olmo. Kadi ya kwanza ya njano ilitolewa dakika ya 40 baada ya Lisandro Martinez kumuangusha Oyarzabal, ingawa mlinzi huyo wa Manchester United alitolewa baadaye kutokana na majeraha.
Mchezo ulizidi kuwa mkali katika dakika za nyongeza za muda wa kawaida, ambapo Enzo Fernandez, ambaye tayari alikuwa ameonywa kwa kadi ya njano, alipata kadi ya pili ya njano kwa kumchezea vibaya beki wa Hispania Pau Cubarsi na hivyo kutolewa nje.
Mlinda lango wa Argentina Emiliano Martinez aliendelea kuwa tegemeo la timu yake alipookoa kwa ustadi mkubwa mpira wa adhabu wa Lamine Yamal katika sekunde za mwisho za muda wa kawaida. Pia aliokoa kichwa cha Nico Williams katika muda wa nyongeza, lakini baadaye Williams alifunga bao ambalo lilikataliwa kutokana na Mikel Merino kumfanyia madhambi Nicolas Otamendi wakati wa kutengeneza shambulizi.
Argentina ilikuwa imeonesha uwezo mkubwa kwa kugeuza matokeo dhidi ya Misri na England katika hatua za mtoano, lakini haikuweza kufanya hivyo tena dhidi ya Hispania.
Kwa ushindi huo, Hispania ilitwaa Kombe la Dunia la wanaume kwa mara ya pili katika historia yake.
Aidha, ushindi huo uliifanya Hispania kuwa taifa la kwanza kabisa katika historia kushikilia ubingwa wa Kombe la Dunia la wanaume na wanawake kwa wakati mmoja.
Unaweza kusoma;