Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesema nchi yake ipo katika “vita kamili” na Marekani.
Pezeshkian amesisitiza kuwa vita vya sasa havihusishi makombora pekee bali pia uchumi na maisha ya wananchi.
Aidha, amesema Marekani imeshindwa kuilazimisha Iran kujisalimisha kupitia mashambulizi ya kijeshi na sasa inaendesha vita vya mseto vinavyolenga uchumi na ustawi wa wananchi wa Iran.
Katika hatua nyingine, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baghaei, amesema nchi hiyo imepokea mapendekezo kutoka kwa wapatanishi huku mashambulizi ya kulipizana kati ya Tehran na Washington yakiendelea.
Baghaei amesema Iran inaendelea na juhudi za kidiplomasia sambamba na majibu yake ya kijeshi dhidi ya mashambulizi ya Marekani.
Kuhusu Mlango wa Hormuz, amesema Iran itaendelea kutumia mamlaka yake juu ya njia hiyo muhimu ya maji na kuzuia matumizi yoyote yanayoweza kuhatarisha maslahi yake.
Katika wiki moja iliyopita, Marekani imefanya mashambulizi kadhaa katika kusini mwa Iran, ikisema yanalenga kupunguza uwezo wa Tehran wa kutishia usafirishaji wa kibiashara baharini. Iran nayo imejibu kwa mashambulizi ya makombora na ndege zisizo na rubani dhidi ya vituo vya kijeshi vya Marekani katika nchi Kuwait, Bahrain na Jordan.