Nchini Kenya, mahakama inaanza kuchunguza rufaa leo Jumanne Julai 21, ikitaka kusimamisha makubaliano muhimu ya madini kati ya Nairobi na Washington. Shirika la utetezi wa maslahi ya umma la Kenya,  Centre for Litigation Trust, linalaani mradi huo, uliojadiliwa kwa siri bila kushauriana na umma wala bunge, karibu na Mrima Hill katika Kaunti ya Kwale, eneo lenye madini mengi ya ardhi adimu lakini pia lenye ulinzi.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Chini ya vilima vyenye misitu vya Mrima Hill kuna madini yanayotumika katika kila kitu kuanzia ndege na roketi hadi miundombinu na mabomba ya mafuta. Eneo hili la karibu hekta 160 lina akiba kubwa ya adhi adimu na madini ya kimkakati.

Lakini Mrima Hill pia ni msitu unaolindwa, mnara wa kitaifa, na eneo takatifu kwa jamii za Kaya za eneo hilo. Sheria ya Kenya kwa ujumla inapiga marufuku shughuli za uchimbaji madini katika minara ya ukumbusho ya kitaifa.

Kwa hivyo, uchimbaji wake unaoowezekana chini ya makubaliano na Marekani yana utata. “Hakuna anayejua masharti ya mkataba,” anaelezea Patrick Ochieng, mwanachama wa shirika la Centre for Litigation Trust, shirika lililo nyuma ya hatua hii ya kisheria. “Hakuna aliyeona tathmini ya athari za mazingira. Hakuna anayejua mipango ya umiliki, mpango wa kugawana faida, au maeneo yatakayoathiriwa. Kwa mradi unaoathiri eneo lenye umuhimu wa kiikolojia na kitamaduni, wengi walitarajia idhini ya bunge.”

Zaidi ya mradi wa madini pekee, kupingwa huku kunaonyesha kutokuaminiana kunakoongezeka kuhusu jinsi baadhi ya mikataba  inavyohitimishwa na serikali, hasa makubaliano ya afya na kituo cha karantini cha Marekani kwa ajili ya Ebola. “Wakenya hawahoji thamani ya mipango hii, bali jinsi inavyotekelezwa,” anaelezea Johnpaul Omollo, mtaalamu wa sera za umma. “Mikataba mingi inaonekana kujadiliwa kwa siri, ingawa Katiba inawahakikishia raia haki ya kupata taarifa.”

Kutokana na ukosefu huu wa uwazi, raia na mashirika ya kiraia wanazidi kugeukia mahakamani kukumbusha serikali kuhusu wajibu wake wa kuheshimu Katiba.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *