Aurélien Tchouaméni

Chanzo cha picha, Getty Images

Iliyochapishwa

Muda wa kusoma: Dakika 3

Real Madrid wako tayari kumuuza kiungo wa ulinzi wa Ufaransa Aurélien Tchouaméni (miaka 26) iwapo Manchester United watatoa ofa inayokubalika. (The Sun)

Manchester United pia wanawafuatilia kiungo wa AS Roma, Manu Koné (miaka 25), na kiungo wa Brighton, Carlos Baleba (miaka 22), ili kuimarisha safu yao ya kiungo. (Sky Sports)

Kiungo wa Bournemouth na timu ya taifa ya Marekani, Tyler Adams (miaka 27), anayekadiriwa kuwa na thamani ya takribani pauni milioni 35, pia ni miongoni mwa wachezaji wanaotazamwa. (Daily Mail)

Adams

Chanzo cha picha, Getty Images

Arsenal wanawawinda mabeki wa England John Stones wa Manchester City na Ezri Konsa wa Aston Villa, kufuatia jeraha la beki wao wa Ufaransa William Saliba. (Sky Sports)

Chelsea wanaongoza mbio za kumsajili kiungo mshambuliaji wa Bosnia na Herzegovina Kerim Alajbegovic kutoka Bayer Leverkusen. Wakati huohuo, Leverkusen pia wanafanya mazungumzo na Crystal Palace kuhusu kumuuza beki wa kati wa Ufaransa Axel Disasi. (The Telegraph)

Chelsea wamekubaliana kumsajili winga wa Marekani Benji Flowers kutoka FC Dallas, ambapo atajiunga rasmi atakapofikisha umri wa miaka 18. (The Athletic)

Arsenal na Manchester City ni miongoni mwa vilabu vinavyowania saini ya winga wa Ivory Coast Yan Diomande wa RB Leipzig, ambaye awali alikataliwa ofa ya pauni milioni 69 kutoka Liverpool. (Bild)

Yan Diomande

Chanzo cha picha, Getty Images

Beki wa Liverpool na timu ya England chini ya miaka 20, Amara Nallo, anatarajiwa kujiunga na klabu ya Finland HJK Helsinki kwa mkopo wa msimu mmoja. (The Athletic)

Mshambuliaji wa Celtic na Japan, Daizen Maeda, anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya Ijumaa kabla ya kukamilisha uhamisho wa pauni milioni 10 kwenda Ipswich Town. (Sky Sports)

Winga wa Leeds United, Jack Harrison , anakaribia kuhamia klabu ya Marekani New England Revolution inayoshiriki Ligi Kuu ya Marekani (MLS). (The Athletic)

Everton wanavutiwa na beki wa kulia wa Celtic, Alistair Johnston, baada ya kuvutia akiwa na timu ya taifa ya Canada katika Kombe la Dunia. (Daily Record)

Aston Villa wanataka kumsajili kiungo wa Everton na England, James Garner, katika dirisha hili la usajili. (Football Insider)

Kocha wa Manchester City, Enzo Maresca, bado ana nia ya kuwasajili kiungo wa Argentina Enzo Fernández na beki wa kulia wa Ufaransa Malo Gusto kutoka klabu yake ya zamani, Chelsea. (CaughtOffside)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *