Takaichi

Chanzo cha picha, Reuters

Mamilioni nchini Japani wanapiga kura katika uchaguzi wa ghafla ulioitishwa na Waziri Mkuu Sanae Takaichi, ambaye muungano wake unatabiriwa kupata ushindi mkubwa.

Miezi michache tu baada ya kuchaguliwa na wabunge, Takaichi aliamua kwenda kwenye vituo vya kupigia kura ili kutafuta mamlaka ya umma.

Kura za maoni zinaonesha kuwa muungano wa Chama chake cha Liberal Democratic Party (LDP) na Japanese Innovation Party chenye wafuasi wengi unaweza kupata hadi viti 300 kati ya 465 katika Bunge la Chini, na kuashiria mabadiliko ya chama cha LDP ambacho kilipoteza udhibiti wa vyumba vyote viwili vya bunge la Japani mwaka jana.

Kiongozi huyo wa kihafidhina amewashawishi baadhi ya wapiga kura kwa kutoa punguzo la kodi na ruzuku, lakini wakosoaji wanasema hili litakuwa pigo kubwa kwa uchumi unaodorora wa Japani.

Karibu watu milioni 4.6 walikuwa wamepiga kura mapema kufikia wiki moja iliyopita, ikiwa ni chini ya 2.5% kutoka uchaguzi uliopita wa 2024, huku kushuka huko kukiwa kunahusishwa na theluji kubwa katika maeneo ya kaskazini na magharibi.

Waangalizi wanasema umaarufu binafsi wa Takaichi unaweza kusaidia kuongeza ufanisi wa chama cha LDP katika uchaguzi huu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *