
Mwandishi maalum wa Umoja wa Mataifa amesema siku ya Alhamisi huko Geneva kwamba dunia imeingia katika “enzi mpya ya unyanyasaji” kwa jina la mapambano dhidi ya ugaidi, ambayo amesema Marekani inayatumia “kuchochea vurugu na maafa” nchini Iran na Venezuela.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Vita katika Mashariki ya Kati, vilivyoznduliwa Februari 28 na mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran, havitaboresha usalama wa dunia, alisema Ben Saul, Mwandishi Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu na kupambana na ugaidi, katika mkutano na waandishi wa habari. “Tumeingia katika enzi mpya ya unyanyasaji kwa jina la mapambano dhidi ya ugaidi,” alilalamika. “Hivi majuzi, imehalalisha uchokozi wa moja kwa moja na kuibuka tena kwa ubeberu dhidi ya Iran na Venezuela, kuchochea vuruu na maafa, kukiuka haki ya kuishi, na kuifanya dunia kutokuwa na usalama hata kidogo,” Ben Saul aliongeza.
Ben Saul pia alikosoa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kupitisha azimio siku ya Jumatano “ambalo lilishindwa kulaani uchokozi wa Israel na Marekani,” huku akilaani “badala yake jibu la kupita kiasi na kinyume cha sheria la Iran … Hakuna anayejua jinsi hili litakavyoisha, na tukizingatia hatua za hivi karibuni zilizoongozwa na Marekani nchini Libya, Iraq, Afghanistan – zote zimekuwa majanga,” Mwandishi Maalum alisema.
Waandishi Maalum ni wataalamu huru walioagizwa na Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kutoa ripoti kuhusu uchunguzi wao, lakini hawazungumzii kwa niaba ya Umoja wa Mataifa.