
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ameiambia CNN, katika sehemu ya mahojiano yaliyorushwa siku ya Jumamosi, kwamba Urusi inaipa Iran ndege zisizo na rubani za Shahed zinazokusudiwa kutumika dhidi ya Marekani na Israel.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Ndege zisizo na rubani za Shahed zimehusishwa katika mashambulizi mengine dhidi ya nchi kadhaa katika eneo hilo, ingawa utambulisho wa wmakapuni yaliyotengeneza ndege hizohaujabainishwa wazi.
Iran ilikuwa nchi ya kwanza kutengeneza ndege zisizo na rubani za Shahed, njia mbadala ya bei nafuu zaidi ya makombora ya gharama kubwa. Matumizi yake mengi yalianza wakati wa uvamizi wa Urusi nchini Ukraine, ambapo maelfu ya ndege zisizo na rubani zimezinduliwa na vikosi vya Urusi tangu msimu wa vuli wa 2022, kulingana na mamlaka ya Ukraine.
Ingawa Iran hapo awali ilitoa ndege hizo zisizo na rubani, Urusi sasa inatengeneza ndege zake za Shahed.
Tangu wakati huo, vikosi vya jeshi vya nchi zingine vimetumia ndege zisizo na rubani za aina ya Shahed, haswa jeshi la Marekani, ambalo limesema kwamba ni sehemu ya kampeni ya sasa dhidi ya Iran.
Waziri Mkuu wa Uingereza Starmer anaweza kutuma maelfu ya ndege zisizo na rubani Mashariki ya Kati, kulingana na Telegraph
Wakati huo huo Gazeti la Telegraph linaripoti kwamba maafisa wa kijeshi wanafikiria kutumia mfumo wa ndege zisizo na rubani wa “Octopus” uliotengenezwa Uingereza, uliotengenezwa kwa ajili ya Ukraine kupambana na Urusi, ili kuimarisha ulinzi wa Uingereza dhidi ya ndege zisizo na rubani za Iran.