Wakati Tanzania ikiendeleza safari yake kuelekea mustakabali endelevu na imara, upatikanaji wa nishati safi, ya kuaminika na nafuu umeendelea kuwa moja ya nguzo muhimu za maendeleo ya Taifa.
Sambamba na Dira ya Taifa na utekelezaji wa Lengo la Maendeleo Endelevu namba 7 (SDG 7), kampuni bunifu za ndani zina mchango mkubwa katika kubadilisha namna nishati inavyozalishwa, kusambazwa na kutumika nchini.
Moja ya kampuni zilizo mstari wa mbele katika mabadiliko haya ni SEPON LTD, kampuni ya uhandisi wa nishati jadidifu iliyojikita katika kutoa suluhisho bora za nishati zinazoweza kupatikana kwa urahisi katika sekta za makazi, biashara, viwanda na kilimo.
Kuunga mkono dira ya Tanzania ya nishati safi
Serikali ya Tanzania imeweka msisitizo mkubwa katika kuongeza matumizi ya nishati safi na ya kisasa kupitia Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi, unaolenga kufikia asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati safi ifikapo mwaka 2034.
Ingawa matumizi ya nishati safi kwa kupikia ni sehemu muhimu ya mabadiliko haya, mfumo mpana wa nishati safi unajumuisha pia upatikanaji wa umeme, matumizi yenye tija ya nishati, pamoja na miundombinu endelevu.
Kupitia ubunifu wa nishati ya jua, SEPON LTD inachangia katika mfumo huu kwa kubuni na kutekeleza mifumo ya umeme wa jua inayohudumia kaya, biashara, mashamba na taasisi mbalimbali nchini.
Kutoa suluhisho bora za nishati ya jua
Kutokana na Tanzania kuwa na rasilimali kubwa ya mwanga wa jua, teknolojia ya nishati ya jua ni mojawapo ya njia bora zaidi za kupanua upatikanaji wa nishati huku ikipunguza utegemezi wa mafuta.
SEPON LTD inajihusisha na matumizi mbalimbali ya nishati ya jua, ikiwemo; mifumo mseto ya sola (solar hybrid photovoltaic) kwa makazi, biashara, taasisi na majengo ya viwanda, mifumo ya kusukuma maji kwa kutumia sola kwa ajili ya umwagiliaji.
Teknolojia ya joto la sola (solar thermal) kama mifumo ya kupasha maji moto (inayoweza kupunguza gharama za umeme hadi asilimia 65), matumizi ya sola kwa shughuli za uzalishaji vijijini, taa za barabarani na miundombinu ya taa zinazotumia sola, ushauri wa kitaalamu wa masuala ya nishati na usanifu wa mifumo.
Mitambo ya umeme wa jua ikiwa imefungwa katika maeneo ya vijijini kwa ajili ya kuzipatia nishati ya umeme jamii zilizombali na huduma hiyo.
Kupitia suluhisho hizi, SEPON LTD inawezesha jamii na biashara kupata umeme wa uhakika huku wakipunguza gharama na athari kwa mazingira.
Kuleta mapinduzi ya kilimo kupitia nishati ya jua
Kilimo kinaendelea kuwa uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania, lakini wakulima wengi wanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa maji na nishati ya uhakika.
SEPON LTD imekuwa ikitekeleza miradi ya kufunga mifumo ya kusukuma maji kwa kutumia sola inayowawezesha wakulima kumwagilia mazao bila kutegemea jenereta za dizeli zenye gharama kubwa au umeme wa gridi usiotabirika.
Mifumo hii inasaidia wakulima; kuongeza uzalishaji wa mazao, kupunguza gharama za uendeshaji, kupanua shughuli za kilimo, kuimarisha ustahimilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na kuendeleza kilimo endelevu.
Suluhisho hizi sio tu zinaboresha maisha ya wakulima bali pia zinachangia usalama wa chakula na ukuaji wa uchumi wa vijijini.
Nishati safi kwa biashara na jamii
Mbali na sekta ya kilimo, biashara za kisasa nchini zinahitaji suluhisho za nishati zinazohakikisha uhakika na uthabiti wa gharama kwa muda mrefu.
SEPON LTD hutoa mifumo mseto ya sola inayochanganya nishati ya jua, uhifadhi wa betri na miundombinu ya gridi iliyopo, hivyo kuhakikisha upatikanaji wa umeme usiokatika kwa shughuli muhimu.
Mifumo hii ni muhimu sana kwa; hoteli na sekta ya utalii, majengo ya kibiashara, taasisi za afya, shule na vyuo pamoja na viwanda. Nishati safi ya uhakika huongeza ufanisi wa uendeshaji na kusaidia Tanzania kuelekea uchumi wa kijani.
Katika sekta ya afya, mifumo hii inawezesha; uendeshaji endelevu wa vifaa muhimu vya tiba, mifumo ya ya uhakika ya viyoyozi kwa wagonjwa, umeme thabiti kwa maabara na huduma za uchunguzi na kupunguza utegemezi wa jenereta za dizeli
Suluhisho hizi zinawezesha vituo vya afya kufanya kazi kwa ufanisi huku zikishusha gharama za nishati na kuboresha huduma. Kwa vituo vya kisasa vya afya, nishati ya uhakika si anasa bali ni hitaji la msingi.
Kampuni ya Kitanzania yenye maono ya kitaifa
Kama kampuni ya Kitanzania ya nishati jadidifu, SEPON LTD inaamini kuwa utaalamu wa ndani na ubunifu ni msingi wa kujenga mustakabali endelevu wa nishati.
Kwa kuunganisha ujuzi wa uhandisi, uzoefu wa vitendo na dhamira ya dhati ya kulinda mazingira, kampuni inaendelea kusaidia miradi inayokuza upatikanaji wa nishati safi nchini.
Aidha, SEPON LTD imejikita katika kutoa elimu kwa umma kuhusu faida za nishati jadidifu na kuunga mkono jitihada za kitaifa za kuongeza matumizi ya nishati safi.
Mtazamo wa baadaye
Mabadiliko ya Tanzania kuelekea nishati safi yanafungua fursa kubwa za ubunifu, uwekezaji na ukuaji shirikishi wa uchumi.
Kampuni kama SEPON LTD zitaendelea kushirikiana na jamii, wafanyabiashara na wadau wa kitaifa kubuni suluhisho zinazofanya nishati safi iwe rahisi kupatikana, ya kuaminika na nafuu.
Kwa kutumia nishati ya jua, Tanzania hailindi mazingira yake tu bali pia inawezesha wananchi wake na kuimarisha uchumi wao.