Kamandi Kuu ya Jeshi la Iran imeamuru kufungwa Mlango-Bahari wa Kistratejia wa Hormuz muda mfupi baada ya kuanza hujuma mpya ya kijeshi ya Marekani dhidi ya Iran, licha ya Jamhuri ya Kiislamu kuonya juu ya chokochoko hizo.

“Kuanzia sasa, kutokana na ukosefu wa usalama katika Ghuba ya Uajemi; Mlango wa Bahari wa Hormuz umeamriwa kufungwa kwa ajili ya meli zote, ikiwa ni pamoja na meli za mafuta na meli za kibiashara, na meli yoyote itakayojaribu kupita italengwa,” imebainisha taarifa ya Makao Makuu ya Khatamul Anbiyaa leo Alhamisi.

Kamandi Kuu ya Jeshi la Iran imesema kuwa kuwa kuwa amri hiyo imetolewa “kufuatia vitendo vya uchokozi vinavyoendelea kufanywa na mtenda jinai Marekani na kwa kuzingatia kuanza mashambulizi ya jeshi vamizi la nchi hiyo dhidi ya maeneo kadhaa katika mkoa wa kusini wa Hormozgan.”

“Tunayakadhibisha madai ya Marekani kwamba meli zinapita katika Mlango Bahari huo”, imeongeza taarifa ya Kamandi Kuu ya Jeshi la Iran.

Katika onyo lisilo na shaka, Kamandi Kuu ya Jeshi la Iran pia imesisitiza kuwa “Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu vitatoa jibu kali na madhubuti kwa uchokozi wowote na hatua za kiuhasama za jeshi la vamizi na kigaidi la Marekani katika eneo.”

Wakati huo huo Kikosi cha Wanamaji la Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kimetoa taarifa tofauti na kutangaza kuwa kikosi hicho kimezigonga meli mbili zilizokuwa zikijaribu kuvuka katika njia hiyo ya majini kinyume cha sheria.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *