
Katika taifa ambalo watu wanazungumza lugha nyingi kama Uganda, ambapo kuna lugha zaidi ya 40 zinazungumzwa kote nchini, ni wazi kuwa ni njia ambayo lugha inaweza kuimarisha au kudumaza mafanikio.
Mgombea urais Mubarak Munyagwa amezua taharuki kwa kupendekeza kuondoa lugha ya Kiswahili katika orodha ya lugha za taifa na badala yake kutumia lugha ya Kifaransa.
Ahadi yake, ikiwa ni hatua ya kwenda na wakati, inapuuza utamaduni na kudharau urithi wa Uganda na nafasi yake katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Kwa Uganda, Swahili siyo lugha tu; ni njia ya kuleta mafanikio ya kiuchumi na amani, na kufanya pendekezo la kutumia Kifaransa kuwa lisilo na msingi.
Kiuchumi, Kiswahili hakiwezi kubadilishwa na chochote. Uganda, ni nchi ambayo kimkakati uchumi wake unakuwa Afrika Mashariki, na imejumuishwa vizuri, ikiwemo Kenya, Tanzania, Rwanda, Burundi, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Lugha inayotumika katika kanda
Kiswahili ni lugha ambayo inatumika sana, inazungumzwa na watu zaidi ya milioni 200 kote katika kanda. Ni lugha ambayo inatumika katika masoko ya Nairobi, makubaliano ya kidiplomasia mjini Arusha, na biashara kutoka nchi moja hadi nyingine ambayo inasaidia kusafirisha kahawa ya Uganda, dhahabu, na bidhaa za kilimo.
Ufahamu wa lugha ya Kiswahili hausaidii katika kuchagiza biashara tu; inafungua uwekezaji, utalii, na ajira.
Juhudi za Uganda kufanya Kiswahili kuwa somo shuleni tangu 1992, zinadhihirisha hili.
Uganda ni koloni la zamani la Uingereza, siyo Ufaransa; Kiingereza tayari kinatumika zaidi ulimwenguni. Kulazimisha raia wa Uganda kuzungumza Kifaransa kutawafanya watengwe, kwa kuwafanya wajifunze lugha ambayo inawaweka mbali na shughuli zao za kila siku na majirani zao.
Kiswahili, lugha ambayo asili yake ni lugha za Kibantu kinazungumzwa na mamilioni ya watu nchini Uganda—kutoka lugha ya Luganda hadi Runyankole.