Rais Donald Trump ameonya kuwa Marekani inaweza kufanya mashambulizi mengine ya anga nchini Nigeria ikiwa mauaji ya Wakristo yataendelea.

Katika mahojiano na gazeti la New York Times, lililochapishwa siku ya Alhamisi, Bw Trump aliulizwa ikiwa mashambulizi ya hivi majuzi ya anga ya Marekani katika jimbo la Sokoto nchini Nigeria yakilenga wanamgambo wa wenye itikadi kali yalikuwa sehemu ya operesheni kubwa zaidi ya kijeshi.

Akijibu swali hilo, Trump alisema: “Ningependelea liwe shambulio la mara moja.” Hata hivyo, aliongeza kwa msisitizo: “Iwapo mauaji dhidi ya Wakristo yataendelea, basi yatakuwa mashambulizi ya mara kwa mara.”

Utawala wa Trump hapo awali umeikosoa vikali serikali ya Nigeria kwa kile ilichokitaja kuwa kushindwa kuwalinda Wakristo dhidi ya mashambulizi ya wanamgambo wa jihadi.

Aidha, utawala huo umedai kuwa kinachoendelea nchini humo ni aina ya “mauaji ya kimbari”.

Shambulio la anga lililofanywa na Marekani lilitekelezwa usiku wa Krismasi, wiki chache baada ya Rais Trump kutoa onyo kuwa angechukua hatua dhidi ya Nigeria kufuatia madai hayo.

Hata hivyo, serikali ya Nigeria imekanusha madai hayo, ikieleza kuwa hali ya ukosefu wa usalama nchini humo inawaathiri wananchi wa dini zote, na kwamba vurugu hizo hazilengi Wakristo pekee.

Kufuatia hali hiyo, Nigeria imeendelea kuimarisha ushirikiano wake wa kiusalama na Marekani. Akizungumza na BBC, Waziri wa Mambo ya Nje wa Nigeria, Yusuf Maitama Tuggar, alisema kuwa shambulio la usiku wa Krismasi lilikuwa ni “operesheni ya pamoja” na halikuhusishwa na dini yoyote maalum.

Kwa upande wao, maafisa wa serikali ya Nigeria walisema kuwa shambulio hilo lilitekelezwa kwa “idhini kamili” ya Rais Bola Ahmed Tinubu, likishirikisha kikamilifu majeshi ya ulinzi na usalama ya Nigeria.

Baada ya mashambulizi hayo ya anga, Waziri wa Vita wa Marekani, Pete Hegseth, aliandika ujumbe kwenye mtandao wa X akisema, “Mengine yanakuja,” huku akitoa shukrani kwa serikali ya Nigeria kwa msaada na ushirikiano wake.

Hata hivyo, b

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *