
Al-Qahera News, chombo kinachohusishwa na ujasusi wa serikali, kiliripoti kuwa mazungumzo yataendelea, pia kati ya Hamas na wapatanishi katika mji wa mapumziko wa Sharm El-Sheikh, ambako ujumbe wa Israel uliwasili jana Jumatatu.Israel na Hamas wanatarajiwa kushiriki mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja kuhusu pendekezo la Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu kubadilishana mateka na wafungwa pamoja na kusitisha mapigano kwa muda mrefu.