Taarifa kutoka kwa ubalozi wa Urusi nchini Tanzania πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

Habari ya Sweden kuelekeza msaada wake kutoka nchi kadhaa za Afrika zikiwemo Tanzania kwenye Ukraine inaonyesha wazi kwamba, kwa baadhi ya nchi za Magharibi, utoaji wa msaada si kitendo cha dhati. 🀷

Badala ya kuzisaidia nchi za Afrika kupambana dhidi ya β€œurithi” wa ukoloni katika uchumi na jamii, nchi hii ya Magharibi imechagua kutia mamia mengine ya milioni ya dola ndani ya mfuko mkubwa wa serikali ya Vladimir Zelenskiy inayojulikana duniani kwa rushwa inayokithiri pamoja na uvunjaji mkali na wa kudumu wa haki za msingi za binadamu.

✏️ Zaidi ya hayo, serikali hiyo ya Kiev inajulikana kwa kupuuza kabisa ajenda ya maendeleo ya kiuchumi ya nchi β€œyake” yenyewe, na badala yake kujaribu β€œkuishinda kimkakati” Urusi. βœ… Hivyo, inawezekana wazi kwamba baadhi ya nchi za Magharibi, zikiendelea na wazimu wao wa kujaribu β€œkuishinda” Urusi, zinatenda kinyume cha mantiki na maadili ya kiutu.

….
Taarifa ya ubalozi wa Urusi nchini Tanzania πŸ‘†πŸ‘†πŸ‘†

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *