Mvua kubwa ya theluji na hali ya hewa ya barafu imesababisha usumbufu mkubwa wa usafiri kote Ulaya, huku watu sita wakiripotiwa kufariki katika matukio yanayohusiana na hali ya hewa hiyo barani humo.

Watu watano walifariki katika maeneo mawili tofauti ya Ufaransa kutokana na hali mbaya ya hewa wakati wakiendesha gari, mamlaka zimesema, huku mwanamke mmoja pia akifariki katika mji mkuu wa Bosnia, Sarajevo, baada ya theluji ya inchi 16 (sentimita 40) kumuangukia.

Mamia ya safari za ndege zimefutwa kote Ulaya, huku maelfu wakiwa wamekwama katika viwanja vya ndege vya Paris na Amsterdam.

Usumbufu unatarajiwa kuendelea hadi Jumatano.

Nchini Ufaransa, watu wengine watatu walifariki katika matukio mawili tofauti huko Landes, kusini-magharibi, kutokana na barafu, mamlaka zinasema.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *