Tarehe yalLeo, Aprili 2, 2026, ndio namalizika rasmi muhula wa Mohamed Bazoum. Rais huyo wa Niger alipinduliwa katika mapinduzi ya kijeshi mnamo Julai 26, 2023. Miaka miwili na nusu baadaye, yeye na mkewe bado wanazuiliwa Niamey. Wito wa kuachiliwa kwake unaendelea kutolewa.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Mohamed na Khadiza Bazoum bado wanazuiliwa katika moja ya makazi ya rais, ambapo hawawezi kuondoka. Wanazuiliwa na mamlaka ya Niger.

Mazingira ambamo wanazuiliwa hayajabadilika. Hata hivyo, sasa wanaruhusiwa kuwasiliana na watoto wao kila wiki, kulingana na mshirika wa karibu. Ari ya rais aliyeondolewa madarakani ni nzuri.

Mwanzo wa muhula wa Mohamed Bazoum ulikumbwa na jaribio la mapinduzi. Hili lilitokea Machi 31, 2021, siku mbili kabla ya kuapishwa kwake. Hatimaye alipinduliwa miaka miwili baadaye na jeshi, ambalo bado liko madarakani huko Niamey, likiongozwa na Jenerali Tiani.

Tangu wakati huo, majaribio kadhaa ya upatanishi yamefanywa ili kuhakikisha kuachiliwa kwa Mohamed Bazoum, yakiongozwa na Togo, Morocco, na mengineyo. Muungano wa Kimataifa kwa ajili ya Ukombozi wa Mohamed Bazoum ulituma barua ya wazi mnamo mwezi Desemba 2025 kwa taasisi kadhaa za kimataifa, ikitaka uhamasishaji wa haraka wa kimataifa wa kuachiliwa kwa rais wa Niger.

Mnamo mwezi Machi mwaka uliyopita, bunge la Ulaya lilipitisha azimio likitaka kuachiliwa kwake kabla ya muhula wake kumalizika. Mpango huu ulishtmiwa na nchi tatu za ESA, ambazo ziliulaani kama kuingilia masuala ya Niger. Hakuna hata moja ya mipango inayotaka kuachiliwa kwa rais huyo wa zamani ambayo imefanikiwa hadi sasa.

Kinga ya Mohamed Bazoum iliondolewa miaka miwili iliyopita, lakini hakuna kesi rasmi zilizoanzishwa. Chama tawala cha CNSP hakitaji tena, angalau hadharani, hali ya rais huyo aliyeondolewa mamlakani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *