Kwa mujibu wa shirika la habari la serikali ya China, Xinhua, Rais wa China Xi Jinping ameonya kwamba dunia kwa mara nyingine inaelekea kurejea katika “sheria ya msituni (ubabe),” akimaanisha kuwa pasipo kuwepo kwa kanuni za kuongoza ulimwengu, kila jambo linaweza kufanyika bila mipaka.
Kwa mujibu wa shirika hilo, Rais Xi alitoa kauli hiyo wakati wa mazungumzo na mwenzake wa Uhispania, Pedro Sánchez, ambaye yuko katika ziara nchini China.
Akiashiria kinachoonekana kuwa ni vita vinavyoendelea katika Mashariki ya Kati, alisema dunia ipo katika hali ya “vurugu,” na kwamba kuna “mkanganyiko kati ya utekelezaji wa sheria na matumizi ya nguvu.”
Katika mkutano huo, Rais Xi alisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya China na Uhispania ili kuzuia dunia isije ikaangukia katika “sheria ya msituni,” na kulinda “utaratibu wa kimataifa unaozingatia sheria za kimataifa.”
#chanzobbcswahili

(Feed generated with FetchRSS)