Visa vya ugonjwa wa uti wa mgongo unaosababisha vifo unaongezeka mashariki mwa Chad, na kusababisha vifo vya karibu 12% ya watoto walioambukizwa katika eneo hilo, ambalo linahifadhi mamia ya maelfu ya wakimbizi wa vita kutoka nchi jirani ya Sudan, Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) limesema siku ya Alhamisi.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Ugonjwa wa Surua pia unaenea katika mji wa mpakani wa Adré, ambapo ongezeko la wageni katika wiki za hivi karibuni limesababisha msongamano katika kambi, na hivyo kuwezesha kuenea kwa magonjwa, shirika hilo la kibinadamu limesema katika taarifa.

Kati ya watoto 212 waliolazwa katika vituo vya MSF kwa ugonjwa wa uti wa mgongo kati ya mwezi Machi na mwezi Aprili, 25 walifariki, “kiwango cha kutisha cha vifo,” MSF imeongeza. “Kila siku, tunaona watoto wakiwasili hapa na surua kali, pamoja na nimonia, wakihitaji kulazwa hospitalini kwa dharura,” amesema Isabelle Kavira, meneja wa huduma za matibabu wa MSF huko AdrĂ©.

“Idadi ya wagonjwa wa uti wa mgongo iko karibu 100%, na hivyo kuhatarisha uwezo wetu na kuhatarisha huduma kwa magonjwa mengine.”

Zaidi ya wakimbizi milioni 1.3 wa Sudan wanaishi katika nchi jirani ya Chad, kulingana na takwimu za Umoja wa Mataifa, wakiwemo manusura wa mauaji na njaa huko Darfur.

Wengi wamewasili tangu kuanza kwa mzozo nchini Sudan kati ya jeshi na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), mwezi Aprili 2023.

Wizara ya Afya ya Chad na wafanyakazi wa MSF wametoa chanjo za dharura za surua kwa zaidi ya watoto 95,500 na chanjo za ugonjwa wa uti wa mgongo kwa watu 337,800 katika maeneo yaliyoathiriwa zaidi, shirika hili la kibinadamu limeripoti.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *