Papa Leo wa Kumi na Nne, kiongozi wa Wakatoliki duniani, ameendelea kukosoaji vikali sera za kuchochea vita za Donald Trump, Rais wa Marekani, akiwa ziarani barani Afrika na kwa mara nyingine amekemea vita na mashambulizi ya nchi hiyo ikishirikiana na utawala haramu wa Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.

Ripoti ya Shirika la Habari la IRNA ikinukuu New York Times, imesema, akiwa kwenye ndege akirejea nyumbani baada ya kukamilisha ziara yake barani Afrika, Papa Leo amezungumza na waandishi wa habari na kwa mara nyingine amekemea vikali vita dhidi ya Iran.

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani ameeleza masikitiko yake kwamba mzozo huo umesababisha “vifo vya watu wengi wasio na hatia.”

Ameongeza pia kwamba kasi ya mazungumzo ya amani ni ya mwendo wa kinyonga na akasema: “Hatujui mchakato huu ambao umeibua hali ya machafuko kwenye uchumi wa dunia unaelekea wapi.”

Akiwa nchini Algeria, Papa Leo aliwaambia wenye madaraka ya utawala kwamba wanapaswa “kuendeleza jamii ya kiraia iliyo hai, yenye nguvu na yenye uhuru.”

Huko Cameroon, Papa alikutana na “Paul Biya,” mwenye umri wa miaka 93, ambaye ametawala nchi hiyo kwa zaidi ya miongo minne, na akaonya juu ya “kiu ya kipagani ya kujilimbikizia faida.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *