
Utafiti uliofanywa na wataalamu wa shirika la Afya Duniani (WHO) na Chuo cha Imperial unakadiria idadi ya visa kuwa mara mbili hadi tano zaidi kuliko takwimu za sasa.
Imechapishwa:
Dakika 3 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
►Utafiti uliochapishwa Mei 18 na Chuo cha Imperial London, kwa ushirikiano na shirika la Afya Duniani (WHO), unakadiria kuwa mlipuko wa virusi vya Ebola Bundibugyo nchini DRC ni mkubwa zaidi kuliko takwimu rasmi zinavyoonyesha. Mnamo Mei 19, Waziri wa Afya wa Kongo, Roger Kamba, aliripoti wagonjwa 543 wanaoshukiwa kuambukizwa virusi hivyo na vifo 136. Kufikia Mei 16, tarehe ya msingi ya utafiti, mamlaka ziliripoti wagonjwa 336 wanaoshukiwa kuambukizwa virusi vya Ebola Bundibugyo na vifo 88. WHO tayari inashuku mlipuko huo umesababisha vifo 139 kati ya wagonjwa 600 wanashukiwa kuambukizwa virusi hivyo kwa jumla. Kulingana na watafiti hawa, idadi halisi ya watu walioambukizwa ni kati ya 400 na 800, na inaweza kuzidi 1,000. Marekani imeainisha jimbo la Ituri katka kiwango cha 4: watu kutosafiri kutoka mkoa huo kwenda maeneo mengine nchini au nchi jirani.
Hali ilivyokuwa kufikia Mei 20. Tangu kuchapishwa kwa utafiti huo, takwimu zimeendelea kubadilika kwa kasi. Katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Mei 19, Waziri Roger Kamba alitoa takwimu za hivi karibuni: visa 543 vinavyowezekana vilivyotambuliwa katika jamii, vifo 136 vinavyowezekana, wagonjwa 69 walio katika vituo vya matibabu kwa sasa, na visa 32 vilivyothibitishwa na vipimo vya maabara katika INRB (Taasisi ya Kitaifa ya Utafiti wa Biomedical). Waziri alifafanua kwamba takwimu hizi zinatokana na uchunguzi wa kina. Hivi si visa vya Ebola vilivyothibitishwa, lakini visa vinavyoshukiwa, vilivyotambuliwa kulingana na dalili zinazoendana na ugonjwa huo. Maeneo manne ya afya sasa yameathiriwa huko Ituri: Mongwalu, Bunia, Rwampara, na Niakunde. Butembo na Goma pia zimeongezwa kwenye orodha. Kulingana na WHO, janga hilo tayari linashukiwa kusababisha vifo 139 kati ya visa 600 vinavyowezekana kwa jumla.
►Utafiti unasema nini. Utafiti huu umeandaliwa na timu ya kimataifa: watafiti kutoka Chuo cha Imperial London, Programu ya Dharura ya Afya ya WHO huko Geneva, WHO Uganda, WHO DRC, Wizara ya Afya ya Uganda, na Taasisi ya Kitaifa ya Afya ya Umma ya DRC. Chuo cha Imperial ni mojawapo ya taasisi maarufu zaidi duniani katika uundaji wa mifumo ya mlipuko. Wakati wa janga la UVIKO-19, kazi yake ilichochea maamuzi ya serikali kadhaa.
Hitimisho kuu limeundwa kwa uangalifu: kufikia Mei 17, kati ya visa 400 na 800 vya ugonjwa wa virusi vya Bundibugyo vingeweza kuripotiwa nchini DRC. Watafiti wanabainisha kuwa takwimu zinazozidi 1,000 haziwezi kutengwa kutokana na data iliyopatikana wakati huo. Kinachoongeza uzito katika safu hii ni kwamba mbinu mbili huru za hesabu hufikia matokeo sawa.
►Njia mbili, ishara moja ya tahadhari. Njia ya kwanza huanza na ishara rahisi: wagonjwa wawili kutoka Ituri waligunduliwa Kampala, Uganda. Walisafiri kwa ajili ya matibabu. Watafiti walilinganisha hali hii na data ya watu waliotangamana na wagonjwa hao katika vivuko vya mpakani kati ya DRC na Uganda. Huko Ituri, takriban wasafiri 1,871 huvuka mipaka hii kila siku kuingia Uganda. Kulingana na hili, wanakadiria idadi inayowezekana ya visa nchini DRC kuwa kati ya 235 na 470, kulingana na dirisha la utambuzi lililotumika.
Njia ya pili huanza na vifo 88 vinavyoshukiwa kuripotiwa kufikia Mei 16, vinavyochukuliwa kuwa vya kuaminika zaidi kuliko idadi ya visa, kwa sababu kifo ni vigumu kupuuza kuliko mtu mgonjwa anayebaki nyumbani. Kwa kutumia kile kinachojulikana kutokana na milipuko miwili iliyopita ya virusi vya Bundibugyo, wanapata kati ya visa 400 na zaidi ya 1,000, kulingana na kiwango kinachodhaniwa cha kuenea kwa mlipuko huo. Mbinu zote mbili zinafikia hitimisho moja: kutogunduliwa kwa kiwango kikubwa
