s

Chanzo cha picha, Getty Images

Manchester United wameahirisha mazungumzo ya kuongeza mkataba wa nahodha wao na kiungo wa Ureno, Bruno Fernandes, mwenye miaka 31, baada ya kuhakikishiwa kuwa anataka kubaki Old Trafford kwa muda mrefu. (Mirror)

Real Madrid wanatarajiwa kutoa pauni milioni 17.3 ili kumsajili beki wa kulia wa Inter Milan na timu ya taifa ya Uholanzi, Denzel Dumfries, mwenye miaka 30. (Sky Sports)

Everton wanamuwania mshambuliaji wa Brazil wa Arsenal, Gabriel Jesus, mwenye umri miaka 29, lakini wanataka mabingwa hao wa Ligi kuu kupunguza bei yao ya pauni milioni 20. (Football Insider)

s

Chanzo cha picha, Getty Images

Paris Saint-Germain wanataka euro milioni 30 (pauni milioni 25.9) kutoka Juventus kwa ajili ya mshambuliaji wa Ufaransa mwenye miaka 27, Randal Kolo Muani. (La Gazzetta dello Sport)

Atletico Madrid wanaweza kutumia fedha watakazopata kutokana na mauzo ya mshambuliaji wa Argentina, Julian Alvarez, mwenye miaka 26, kumsajili mshambuliaji wa Marseille na England, Mason Greenwood, mwenye miaka 24. (Fichajes)

Roma pia wanamfuatilia Mason Greenwood, huku klabu yake ya zamani Manchester United ikitarajiwa kunufaika kupitia kipengele cha asilimia ya mauzo ya baadaye kilichowekwa wakati wa uhamisho wake kwenda Ufaransa. (Teamtalk)

AC Milan wanamtaka Crysencio Summerville, mwenye umri wa miaka 24, kutoka West Ham United. Winga huyo wa Uholanzi pia anafuatiliwa na Tottenham Hotspur na Aston Villa. (Teamtalk)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *