Wakala wa Barabara nchini, TANROADS imesitisha kwa muda matumizi ya sehemu ya barabara kuu ya Morogoro-Singida … katika eneo la CBE na mataa ya Chako ni Chako lililoko katikati ya mji wa Dodoma, baada ya mvua zinazoendelea kunyesha kusomba udongo chini ya barabara na kusababisha shimo kubwa linalohatarisha usalama wa watumiaji wa barabara hiyo.
Inaelezwa kuwa shimo hilo limeungana na mfereji mkuu wa maji taka uliopo chini ya barabara hiyo, hali iliyosababisha mamlaka husika kuanza kufanya tathmini ya haraka kwa ajili ya ukarabati.
Akizungumza kuhusu hali hiyo, Meneja wa TANROADS Mkoa wa Dodoma, Zuhura Amani, amewataka watumiaji wa barabara kufuata maelekezo ya kutumia njia mbadala zilizotolewa ili kuendelea na safari zao wakati matengenezo yakitarajiwa kuanza.
#AzamTVUpdates
✍George Mbara
Mhariri | John Mbalamwezi
(Feed generated with FetchRSS)