WHO yatangaza mlipuko wa Ebola nchini DR Congo kuwa dharura ya kiafya dunianiWHO yatangaza mlipuko wa Ebola nchini DR Congo kuwa dharura ya kiafya duniani

Raia mmoja wa Canada aliyesafiri kwa meli ya watalii MV Hondius ambayo ilikumbwa na mlipuko wa Hantavirus mwezi Aprili, amepatikana na ugonjwa huo, maafisa wa afya katika jimbo la British Columbia wamesema.

Mtu huyo alikuwa mmoja wa watu wanne waliokuwa wakijitenga katika kisiwa vya Vancouver baada ya kushuka kutoka melini, na alikuwa ameonyesha dalili za kiwango cha chini.

Afisa mkuu wa afya wa jimbo hilo alisema kuwa watu hao wanne hawakuwa wamechangamana na umma tangu walipowasili Canada.

Kisa hicho kinafanya jumla ya maambukizi kufikia watu 11, wote wakiwa abiria wa meli hiyo ya watalii.

Watu watatu waliokuwa wamesafiri kwenye meli hiyo wamefariki dunia, huku wawili wao wakithibitishwa kuwa walikuwa na virusi hivyo.

Afisa wa afya wa British Columbia, Bonnie Henry, alisema matokeo ya vipimo vya mtu huyo yalionesha kuwa ana uwezekano mkubwa wa kuwa na maambukizi ya Hantavirus siku ya Ijumaa, ingawa bado yanahitaji kuthibitishwa na maabara ya kitaifa ya microbiolojia.

“Hili si jambo tulilotarajia, lakini ni jambo tulilokuwa tumejiandaa nalo,” alisema, akikaririwa na shirika la utangazaji la taifa la CBC.

Dkt. Henry aliongeza kuwa: “Ninataka kusisitiza kwamba hantavirus ni virusi tofauti sana na virusi vingine vya mfumo wa upumuaji ambavyo tumekuwa tukikabiliana navyo, na bado hatuoni kuwa vina uwezo wa kusababisha janga la kimataifa.”

Unaweza kusoma;

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *