Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi, amewahimiza wananchi kuzingatia ushauri wa wataalamu wa afya ikiwemo kuzingatia mtindo bora wa maisha kwa kula vyakula vyenye lishe bora, kupunguza matumizi ya pombe na bidhaa za tumbaku pamoja na kujenga tabia ya kufanya mazoezi ili kujikinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza.
Dkt. Samizi ametoa wito huo leo Januari 09, 2026 jijini Arusha wakati akifunga rasmi kambi maalum ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo iliyofanyika katika hospitali ya Arusha, Lutheran Medical Center (ALMC) – Selian, kwa ushirikiano na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).